Miss Tanzania Aingia Kumi Bora Miss World..Endelea Kumpigia Kura ashinde Kabisa

Jana December 10 2014 Watanzania walimpokea kwa shangwe mwakilishi wao kwenye BBAHotshots Afrika Kusini, Idris ambae ndie alitangazwa mshindi wa dola za kimarekani laki tatu siku kadhaa tu baada ya Diamond kuing’arisha Tanzania kwa kushinda tuzo 3 za Channel O.

Good news nyingine ni mshiriki wetu kwenye Mashindano ya Miss World, Happiness Watimanywa ambae saa chache zilizopita imethibitika kwamba ameiwakilisha vizuri Tanzania na kuifanya iingie kwenye kumi bora za mashindano ya Miss World People’s Choice.
Aliandika kwenye instagram “Tanzania Asanteni kwa support na 

uzalendo, tuendelee mpaka namba moja!!!!! #vote #PigaKura 


#DownloadTheApp #MissWorld2014”– @happinesswatimanywa.
Katika list hiyo, Happiness ameshika nafasi ya tisa katika kumi bora kama inavyoonekana hapa chini.

 
Previous
Next Post »