Na:
Meshack Maganga- Iringa
Katika makala zangu
zilizo tangulia nilipoandika kuhusu ujasiriamali nilipata mwitikio kwa kiwango
kikubwa kutoka kwa wasomaji wengi. Baadhi walinitafuta kutaka ushauri wa
mazungumzo ya ana kwa ana kuhusu dhana hii tunayoiita ujasiria mali.
Baadhi ya wasomaji
wameenda mbali sana na kunisisitiza niandike kitabu kinacho husu ujasiriamali,ninapenda kuwaahidi wasomaji wa
Mjengwa Blog kwamba kitabu kipo njiani kinakuja.Tuombe uzima.
Kuna kanuni inayofanya kazi hapa duniani, ipo na
ukubali usikubali ipo, uamini usiamini ipo, uelewe usielewe ipo.
Ukifikiri kuhusu maisha ya hapa
duniani hasa kwa kuangalia mfumo wa maisha kwa kila binadamu tukianzia kwa walemavu,ombaomba,maskini,wagonjwa,vichaa,wanaohangaika
usiku na mchana kwaajili ya chakula tu na nguo za kuficha utupu wao na makundi
mengine lazima utafika mbali sana na kufika mahali na kukubali kuwa kuna kitu
hakijakamilika katika maisha ya hapa duniani.
Au unaweza kuhisi kana kwamba
dunia hii ina mapungufu sana.Najua kwa mwingine anaweza
kusema hayo yote ni mipango ya Mungu na kuishia hapo.
Ukifikifiri tena kuhusu matajiri wa
dunia hii akina Reginald Mengi, Yusuf Manji, Billgates, Carlos Slim,marehemu
Steve Jobs, warren Buffet, Bernard Arnault na Larry Ellison lazima
utajikuta kuwa kuna shida kuelewa hiyo mipango au majaliwa ambayo wengi huamini
kuwa ni ya Mungu kwa watu hawa huwa kama walivyo. Hebu turudi katika
uhalisia wa maisha.
Fikiri kuhusu nchi za Afrika zenye
kila rasilimali zenye utajiri kupita kipimo lakini bado zinashika mkia katika
umaskini duniani, nayo hiyo kama unaamini tuseme ni mipango ya Mungu Juzi,
ijumaa nilikuwa pale Manzese BIG BROTHER,
nikimsubiri rafiki yangu,nilianza kusoma kitabu cha rafiki yangu Tenganamba, ana sema kuwa, katika kuishi kwangu duniani kwa kipindi
kifupi tu nimejikuta napingana na kauli hizo zilizo zoeleka kama: Ng’ombe wa Maskini hazai,
kupata ni majaliwa,asiyekubali kushindwa si mshindani,maisha ni bahati,kisicho
riziki hakiliki, maskini akipata makalio hulia mbwata, na nyingine nyingi
zinazosisitiza kukubali matokeo madogo bila ubishi wowote.
Mfumo na imani potofu kama hizi ndio ulionisukuma mpaka nikaandika makala nyingi kwenye gazeti hili na pia katika mitandao ya kijamii hasa Mjengwablog makala zimenikutanisha na wadau mbalimbali wa ujasiriamali kutoka ndani na nje ya mkoa wa Iringa.
Kutokana na hilo nadiriki kusema kuwa hapa duniani lazima
kuna kanuni inayofanya kazi, haiwezekani binadamu wengine waishi maisha mazuri halafu wengine tukubali kuwa ni mapenzi ya
Mungu wao tu kuwa walivyo wakati wengine kulala chini ya madaraja ya Ubungo
bila chakula.
Kuna kanuni inafanya kazi hapa duniani, ipo na ukubali
usikubali ipo, uamini usiamini ipo, uelewe usielewe ipo .Nilipokuwa nasoma
historia ya watu maarufu duniani kama akina Lincoln, Pluto, Tiger Woods,
Billgates, Einstein, Hugo na wengine nilikubaliana na ukweli kuwa lazima kuna
siri ya kanuni ya kuishi waliyokuwa wanaijua ambayo binadamu wengi duniani
hawaitambui. Sikubali na haiwezekani kuamini kuwa mafanikio yao yalikuja kama
ajali lazima kuna kanuni inayofanya kazi duniani waliijua mapema.
Na huu ukweli inabidi kila binadamu ajue, na kanuni hiyo ipo
ndani ya kila binadamu na kila binadamu anayo.Jamani tuchoke kusikia mafundisho
ya kutumaliza na kutudumaza kiakili kuna siri ya kanuni na hii iwekwe wazi
ijulikane.
Kimsingi,
ujasiriamali Tanzania umeshika kasi miaka ya 2000, hasa kutokana na juhudi za
Serikali ya awamu ya tatu ya Mh. Benjamin Mkapa aliyeruhusu uwekezaji na ndipo
msamiati wa Utandawazi uliposhika kasi na kuboreshwa na sera na sheria
mbalimbali za uchumi kwa mfano, sera ya maendeleo ya biashara ndogo ndogo.
Kutokana na hili, tumeshuhudia watu wengi
wakijitoa kimasomaso kuanzisha biashara au kufanya shughuli mbalimbali za
ujasiriamali. David McClelland ambaye ni mwanasaikolojia kutoka chuo kikuu cha
Havard nchini Marekani aligundua tabia za kisaikolojia zinazojengeka ndani ya
mjasiriamali ambaye amefanikiwa kibiashara. Akifafanua hoja yake msaikolojia
huyo alisema, wajasiriamali waliofanikiwa huwa na hamasa, malengo na huwa
tayari kutumia muda wao kufanya kile anacho kitaka.
Msamiati huu ulianza
kutumiwa kwa mara ya kwanza na mwana uchumi maarufu Richard Cantillon wa
Ufaransa mwaka 1755 na baadaye ulipata mashiko kuanzia miaka ya 1800 ambapo
wafanya biashara wenye mitaji mikubwa “mechants” kutoka Ulaya walipoanza kuzunguka dunia wakitafuta malighafi na madini kwa ajili ya
viwanda vyao binafsi na vile vya makampuni yao.
Katika kipindi cha zama
za kwanza za mawe (Hunter-Gatherer au miaka ya barafu) Jamii iliishi kwa
kutegemea uwindaji na kukusanya matunda,Jamii iliishi katika makundi madogo
madogo ya watu hasa koo zenye nasaba moja. Watu wote walikuwa sawa,iwapo
alitokea mmoja wa Jamii akawa chifu au
mkuu wa kaya bado hakuonesha tofauti yoyote na wenzake,mkuu wa kabila au
chifu hakumiliki mali nyingi na wala hakuwa milionea.
Baada ya kipindi hicho
kikaja kipindi cha Mapinduzi ya kilimo katika kipindi hiki binadamu alianza
kulima na kufuga aliwekeza nguvu zaidi na alipata mafanikio makubwa na
aliyefanya uzembe wa roho na mwili
aliishia kuwa mlalamishi (tunajua kwamba mlalamishi siku zote hupata
ulalamishi).
Kipindi kingine ambacho
ndio kiini hasa cha makala haya ni kile cha ya mapinduzi ya Viwandani kilikuwa
kipindi kutoka karne
ya 18 hadi karne ya 19 ambapo
mabadiliko makubwa katika kilimo, utengenezaji wa bidhaa, uchimbaji wa madini,
na uchukuzi yalikuwa na matokeo makubwa kwa hali ya kiuchumi, kijamii na ya kitamaduni ikianzia Uingereza, na hatimaye
kuenea Ulaya nzima, Marekani ya Kaskazini, na mwishowe Duniani kote. Mwanzo wa
Mapinduzi ya viwanda ulidokeza mabadiliko muhimu katika historia ya kibinadamu;
karibu kila kipengele cha maisha ya kila siku hatimaye yaliathirika kwa njia
fulani.
Mwanzo wa wakati wa mwisho wa Karne ya 18 mabadiliko
katika baadhi ya sehemu za Uingereza yalianza na kazi ambazo hapo awali zilikuwa za mkononi
na uchumi uliotumia wanyama kuendesha kazi kulibadilishwa na uundaji bidhaa
uliotegemea mashine. Ilianza na utumizi
wa mashine katika viwanda
vya nguo, uundaji kwa
mbinu za kutengeneza chuma na kuzidi kutegemea makaa ya mawe yaliyosafishwa.
Upanuzi wa biashara na ujasiriamali uliwezeshwa na
kuanzishwa kwa mifereji, uboreshaji wa barabara na reli. Kuvumbuliwa kwa nguvu
za mvuke kulikowezeshwa
hasa na makaa ya mawe, utumizi mwingi wa gurudumu
la maji na mashine za
nguvu (hasa katika kutengeneza
nguo) kulisisimua
kuongeza kiwango na uwezo wa uzalishaji
mali
Kuundwa kwa vifaa
vya mashine ambavyo
vilikuwa vya chuma pekee katika miongo miwili ya kwanza ya karne ya 19
kuliwezesha kutengenezwa kwa mashine zaidi za kuunda vifaa katika viwanda
vingine. Matokeo yalienea kote katika Ulaya ya
Magharibi na Marekani ya Kaskazini wakati wa karne ya 19, na hatimaye
kuathiri karibu Dunia yote, mchakato ambao unaendelea katika kuenea
kwa viwanda. Athari ya
matokeo kwa jamii ilikuwa kubwa sana.
Mapinduzi ya Viwanda ya Kwanza, ambayo yalianza katika
karne ya 18, yaliingia katika Mapinduzi ya Pili ya Viwanda mnamo mwaka wa 1850, ambapo maendeleo
ya kiteknolojia na kiuchumi yalizidi kuendelea huku meli zinazotumia mvuke, reli, na baadaye katika karne ya 19 injini ya mwako wa ndani na uzalishaji wa nguvu za umeme. Urefu wa Mapinduzi ya Viwanda
unatofautiana na wanahistoria mbalimbali. ITAENDELEA
meshackmaganga@gmail.com
EmoticonEmoticon