MAZIWA NA NAZI KWENYE MAHARAGE NI KINGA KUBWA YA KIUNGULIA

DSC07084
Katika makala iliyopita Nilifundisha namna ya kupoa asidi iletayo kiungulia kwenye maharage,na tuliona kwamba huwezi kutoa asidi(phytic)yote kwenye maharage ila unaweza kuipunguza kwa kiasi kikubwa ili kuepusha kiungulia.Kwa mantiki hiyo basi,bado kuna kiasi kidogo cha asidi kinachobaki,kuna watu wachache ambao hata kiasi hicho kidogo cha asidi hutosha kuwapa kiungulia.
Kuna namna ya kukata Asidi kidogo inayobaki kwenye maharage baada ya kuyaloweka,unaeweza ongeza maziwa au nazi.
DSC07086
Ili kuelewa kwanini maziwa na nazi vinakata asidi iliyopo kwenye maharage,nilazima utambue kwamba  maziwa na nazi  ni BUFFERs(kiingere)buffer ni mchanganyiko wenye asidi na base kwa pamoja. niwarudishe secondary,enzi zile ukiwa kidato cha pili ulijifunza kuhusu acid and base.Naamini mwalimu wako alikwambia base inauwezo wa ku neutrolise acids.Hicho ndicho kinachotokea unapoweka maziwa kwenye maharage,base iliyo kwenye maziwa inakata/ neutrolise ile phytic acid iliyo kwenye maharage.
DSC07085
Mahitaji
Maharage yaliyochemshwa yakaiva
mafuta ya kula
vitunguu maji
Nyanya
vitunguu swaumu
chumvi
Maziwa
Njia
1.Chemsha maharage adi yaive nay awe laini,hakikisha maji yamekauka kabisa kwenye maharage kabla hujaepua jikoni.Maharage yakiiva na kulainika hupasuka yenyewe
DSC07062
  • Usiweke chumvi unapochemsha maharage,chumvi hufanya maharage yawe magumu
2.Katika sufuria,unga kitunguu na nyanya kama kawaida,ila unapoweka nyanya weka na kitunguu swaumu.kaanga adi viive na mafuta na nyanya vitengane ndani ya sufuria.DSC07066
  • Kawaida mafuta huja juu na nyanya hubaki chini.
3.Ongeza maharage na chumvi kwenye nyanya iliyoiva ,geuza na kaanga kwa muda ili nyanya na maharage viungane na kua kitu kimoja.
DSC07068
DSC07070
4.Ongeza maziwa fresh,kisha koroga ili kuchanganya.weka maziwa yakutosha ili kupata  mchuzi wakutosha.maharage hupendeza zaidi yakiwa na mchuzi.Watoto wengi wanapenda mchuzi wa mahage na si maharage yenyewe.
DSC07072
DSC07073
  • Unaweza weka maji na maziwa ,katika hili,tanguliza maji yakishachemka ndipo uweke maziwa na uchemshe zaidi.
5.Wakati maziwa yanachemka,koroga kila mara ili kuhakikisha maharage hayaungui kwa chini.chemsha adi pale utakapoona maziwa yameiva na mchuzi umekua mzito.katika moto wa wastani,isizidi dakika sita.yakiwa tayari epua jikoni,tayari kwa kula.
DSC07074
DSC07078
Maelezo ya ziada
Kama unaamua kutumia nazi,upishi ni kama huu nilioelezea,ila tu pale nilipoatumia maziwa unaweza tumia nazi.
Unapochemsha na kuivisha maharage ,Hakikisha mchuzi au maji yote yamekauka kwenye maharage ,ili kutunza ladha na utamu wa maharage.wengi mnapenda kuacha mchuzi ili muutumie wakati wa kuunga maharage.Unapoongeza mchuzi huo baada ya kuunga,unapunguza nguvu ya maziwa au nazi,na zaidi ya hapo ubaharibu utamu au ladha ya maharage kwani maziwa na nazi huleta ladha nzuri kwenye maharage.
Maharage ni chakula kizuri sana na kitamu,ila kiungulia,gesi tumboni na upishi mbaya unachangia sana watu wengi kutokula maharage,au kutokuyapenda.
DSC07088
Langu mmoja tu,kukufumbua macho,na kama kawaida utendaji ni juu yako.Ipe familia yako maharage bora sio bora maharage.
Previous
Next Post »