Mwanamke mnene washindwa kumpandisha kwenye Gari la wagonjwa



NewsImages/6712334.jpg



Mwanamke mmoja nchini Emarati anayedhaniwa kuwa wenda akawa ndiyo mwanamke mnene zaidi kuliko wanawake wate nchini humo, jana alifikishwa hospitalini kwa tabu baada ndugu na jamaa kushindwa kumpandisha kwenye gari la wagonjwa
 

Mwanamke huyo mwenye kilo 400, wenda akawa ndiyo mwanamke mnene zaidi Emarati, juzi afikishwa hospitali kwa tabu, baada ya yakupatwa na homa kali iliyopelekea hali yake ya afya kuwa tete, ndugu na jamaa wa mwanamke huyo waliamua kumbeleka hospitali, ndipo walipokutana na kibarua kigumu cha kumtoa ndani mwanamke huyo ili kumumpandisha kwenye gari la wagonjwa.

zoezi la kumpandisha mwanamke huyo kwenye gari hilo la waganjwa lilishindikana mpaka ndugu zake wa karibu walipoomba msaada kwa watu wa huduma ya kwanza na kikosi cha zimamoto, mpaka kufikia idadi ya watu 15, ndiyo walifanikiwa kumtoa ndani ya nyumba na kumpandisha kwenye gari hilo.

Kibarua kiliendelea kuwa kigumu walivyotaka kumshusha baada ya kufikika hospitali kwa ajili ya matibabu, watu wa huduma ya kwanza kwa kushirikiana na kikosi cha zimamoto walifanikiwa kumtoa kwenye gari ya wagojwa akiwa kwenye kitanda na kumuingiza hospitalini.

Kazi ilizidi kuwa ngumu pale walipojaribu kumshusha kwenye kitanda cha gari la wagojwa na kushindwa kufanya hivyo, hali iliyowafanya madakri hospitili hapo kumpatia matibabu yote akiwa katika kitanda cha gari la wagonjwa.

Previous
Next Post »