Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi 
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evodi Mmanda Baada ya 
kuwasili mkoani humo.
 Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akizindua 
mpango kabambe mkoani Mtwara na Mkukabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi. 
Halima Dendego.
 Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akikagua 
mfumo wa ukusanyaji wa kodi ya pango la ardhi katika Halmashauri ya 
Mtwara ili kuhakikisha makusanyo ya kodi yanafanyika kwa ukamilifu.
 Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akikagua 
masijala ya ardhi halmashauri ya Manispaa ya Mtwara na kuwataka Maafisa 
Ardhi kuweka kumbukumbu za Hati Miliki za Ardhi katika mpangilio mzuri 
ili kuepusha migogoro ya ardhi..
 Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi akiongea 
na wananchi wa mkoa wa Mtwara katika uzinduzi wa Mpango Kabambe Mkoani 
hapo.
 Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi (wapili 
kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi. Halima Dendego (wakwanza kushoto), 
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evodi Mmanda (wakwanza kulia), Mwenyekiti 
wa CCM Mtwara Ndugu Muhamed Sinani (wapili kulia) wakiwa katika uznduzi 
huo.
 Wananchi wa Mkoa wa Mtwara wakifuatilia Uzinduzi wa Mpango Kabambe (Master Plan) ya Mtwara.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango Miji na Vijiji Bi. Imaculate Senje akizungumza katika Uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Mtwara.
Ndugu Hamza Sikamkono Afisa Mipango Miji Manispaa ya Mtwara akizungumza katika Uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Mtwara.
Waziri
 wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi amefanya 
uzinduzi wa Mpango Kabambe (Master Plan) ya 2015-2035 Mkoani Mtwara . 
Katika shughuli hiyo Mh. Lukuvi aliwataka watendaji wa Mtwara katika 
sekta ya ardhi kwa kwa kushirikiana na ofisi ya mkuu wa mkoa Bi. Halima 
Dendego kuhakikisha kuwa wanafuata Master Plan hiyo ili kuweza kuipanga 
Mtwara na kanda ya kusini yote vizuri hatimaye kufikia Tanzania yenye 
uchumi wa kati na Viwanda.
Katika
 ziara hiyo, mbali na kuzindua mpango kabambe pia alifanya ukaguzi 
katika mifumo ya ukusanyaji wa kodi ofisi za ardhi za halmashauri ya 
manispaa ya Mtwara ili kuhakikisha makusanyo ya kodi ya ardhi 
yanafanyika kwa malengo mahususi.
Aidha,
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi. Halima Dendego akiongea na wananchi mbele ya
 Waziri Lukuvi, alimhakikishia Mheshimiwa Waziri kuwa atasimamia 
utekelezaji wa mpango kabambe kikamilifu kwa maendeleo ya watu wa Mtwara
  na watanzania kwa ujumla.
Katika
 uzinduzi huo Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango Miji na Vijiji, Bi. 
Imaculate Senje ameeleza kuwa uzinduzi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa 
kupunguza au koundoa kabisa tatizo la migogora ya ardhi mkoani mtwara, 
na kuchochoea fursa za uwekezaji, hivyo amewapa rai wananchi wa Mtwara 
kufuata mpango huo kwa maendeleo ya taifa.
Pia
 Ndugu Hamza Sikamkono Afisa Mipango Miji Manispaa ya Mtwara ameeleza 
kuwa dira ya mpango kabambe huo ni kuwa na mji mahiri wenye uchumi wa 
mafanikio ambao hutoa kazi na fursa za kutosha na kuvutia uwekezaji.
Afisa
 huyo ameeleza mpango huo umegusa maeneo ya Naumbu, Mjimwema, Nanguruwe 
na Ziwani ukigusa huduma zote za kijamii ikiwemo shule na hospitali na 
shughuli za kiuchumi yakiwemo maeneo ya viwanda na uwekezaji.
  
 
EmoticonEmoticon