Jeshi la 
Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria 
zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na
 limekuwa likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada 
hizo za kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa 
ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu.
KUPATIKANA NA DAWA ZA KULEVYA [BHANGI]
Jeshi la 
Polisi Mkoa wa Mbeya kuanzia tarehe 30.04.2017 hadi tarehe 01.05.2017 
lilifanya msako katika maeneo Manga, Uyole Jijini Mbeya na maeneo ya 
Kitongoji cha Iponjola, kijiji cha Isuba, kata ya Kisondela, tarafa 
Pakati, Wilaya ya Rungwe. Katika Msako huo uliolenga kukamata watu 
wanaojihusisha na uuzaji, usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya, 
Watuhumiwa 03 walikamatwa wakiwa na dawa za kulevya aina ya Bhangi yenye
 uzito wa Kilogram 35 na Gram 55.
Watuhumiwa waliokamatwa wametambulika kwa majina ya:-
GOODLUCK GEOFREY [16] Mkazi wa Manga Jijini Mbeya
JAMES S/O MWASEBA [22] Mkazi wa Manga Jijini Mbeya
KISA SHABAN [26] Mkazi wa Kasumulu Wilaya ya Kyela
Watuhumiwa ni wauzaji na wasambazaji wa dawa hizo za kulevya na watafikishwa Mahakamani mara baada ya Upelelezi kukamilika.
KUPATIKANA NA NYARA ZA SERIKALI [MENO YA TEMBO]
Mnamo 
tarehe 30.04.2017 majira ya saa 08:30 Asubuhi, Jeshi la Polisi Mkoa wa 
Mbeya lilifanya msako huko katika maeneo ya Uyole, Kata ya Iganjo, 
Tarafa ya Iyunga Jiji na Mkoa wa Mbeya na kufanikiwa kumkamata mtu mmoja
 aliyefahamika kwa jina la MAIKO KIWAGE [39] Mkazi wa Isyesye akiwa na 
vipande vitatu vya meno ya tembo.Mtuhumiwa alikutwa na nyara hizo za 
Serikali ambazo alikuwa amezihifadhi ndani ya nyumba yake na baada ya 
kumkamata na upekuzi kufanya ndipo zilionekana. Ikumbukwe mnamo tarehe 
24.04.2017 huko Kijiji cha Lyangadupa, Kata na Tarafa ya Rujewa, Wilaya 
ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya watuhumiwa wawili walikamatwa wakiwa na meno 
mawili ya Tembo.Upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao mzima 
unaojishughulisha na uwindaji haramu pamoja na biashara haramu ya Nyara 
za Serikali ikiwani pamoja na Meno ya Tembo na Pembe za Faru.Aidha Jeshi
 la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na matukio makubwa ya 
uhalifu pamoja na wahalifu. Jitihada zinaendelea kwa kushirikiana na 
wananchi kuhakikisha Mkoa wetu unakuwa mahala salama. Hata hivyo 
Kumekuwa na tukio 01 la mauaji kama ifuatavyo:-Mnamo tarehe 01.05.2017 
majira ya saa 10:30 Asubuhi huko katika Kijiji na Kata ya Mjele,  Tarafa
  Usongwe, Wilaya ya Kipolisi Mbalizi, Mkoa wa Mbeya, Mtu mmoja ambaye 
amefahamika kwa jina la SIKITU MWAWALA [25] Mkazi wa Kijiji cha Ijenga 
aliuawa kwa kupigwa na kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria 
mkononi na kisha mwili wake kuchomwa moto. Inadaiwa kuwa chanzo cha kifo
 chake ni kipigo kilichotokana na kulipiza kisasi kufuatia marehemu na 
wenzake kuhusika katika tukio la mauaji ya mwanamke aitwaye ZAITUNI 
SAISONI [20] Mkazi wa Kijiji cha Katusi kilichotokea tarehe 25.04.2017 
majira ya saa 11:00 Asubuhi huko katika Kitongoji cha Kitusi, Kijiji na 
Kata Mjele ambaye baada ya kumuua walichukua baadhi ya viungo vyake 
ikiwemo matiti, masikio, macho na ngozi ya paji la uso kwa imani za 
ushirikina.
Marehemu 
alihusika kwenye tukio hilo ambalo walilitenda pamoja na wenzake wawili 
ambao mmoja kati yao amekamatwa na pia mmoja kati ya watuhumiwa ni mume 
wa marehemu ZAITUNI SAISONI aitwaye MATESO WILLISON [30] Mkazi wa Mjele.
Aidha 
katika tukio hilo zilikamatwa bunduki mbili aina ya Gobole na golori 36 
na unga wa milipuko ambazo moja kati ya bunduki hizo ni ya mali ya 
marehemu aitwaye SIKITU MWAWALA na nyingine ni ya mtuhumiwa ambaye 
amekiri kuwa ni ya kwake.
Marehemu 
pamoja na wenzake wametajwa kuhusika katika matukio ya Unyang’anyi wa 
kutumia silaha, utekaji katika eneo la Msangamwelu na Mjele na pia 
wamekuwa wakikodishwa katika matukio ya mauaji.
WITO:
Kamanda 
wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI
 anatoa wito kwa wananchi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi
 na badala yake wajenge tabia ya kuwafikisha watuhumiwa wanaowakamata 
kwa tuhuma mbalimbali katika mamlaka husika kwa hatua zaidi ya kisheria.
 Aidha Kamanda KIDAVASHARI anatoa wito kwa wananchi kuacha mara moja 
kujihusisha na uwindaji haramu, biashara haramu ya meno ya tembo pamoja 
na uuzaji, usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya kwani ni kinyume 
cha sheria.
Imesainiwa na:
[DHAHIRI A. KIDAVASHARI – DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA
 
 
EmoticonEmoticon