Mbunge Bashungwa (CCM) aeleza kwanini jimboni kwake wanaume hawaoi wanawake wazuri


Kutoka Bungeni, wakati jana wabunge wakichangia hotuba ya Wizara ya Maliasili na Utalii iliyowasilisha bajeti yake jana, Mbunge wa Karagwe alisimama na kueleza kero waipatayo wananchi wake kutoka kwa wanajeshi walioko ndani ya jimbo hilo wanaolinda mipaka ya nchi.
Mbunge wa Karagwa Innocent Bashungwa (CCM) akichangia hotuba alisema “Jimboni kwangu watu hawaoi wanawake wazuri kwa sababu wanachukuliwa na wanajeshi.” Aliitaka wizara husika kuingilia kati suala hili linakalovunja uhuru wa wananchi wa jimboni kwake.
Aidha Mbunge Innocent Bashungwa ameiomba Serikali kuhakikisha inaimarisha ulinzi kwenye kata ya Bweranyangi ambako wanajeshi wengi hulinda mpaka wa nchi ili wananchi waoishi jirani na maeneo hayo waweze kuwa salama na kutimiza majukumu yao ya kila siku kama wananchi wa maeneo mengine.
Previous
Next Post »