Akifungua mkutano huo unaofanyika kwa siku tatu jijini Mwanza, rais
Kiwete amesema kuwa hivi sasa jamii imekuwa na mwamko mkubwa katika
kuhakikisha kuwa kunakuwepo na dhana ya utawala bora, sanjari na suala
zima la uwajibikaji na uwazi katika utumishi wa umma bila kuisahau idara
ya mahakama.
Awali rais wa chama cha mahakimu na majaji wa Afrika Masharika Mh.
Jaji Lawrence Gidudu pamoja na rais wa chama cha mahakimu na majaji
Tanzania Mh. Jaji Ignas Kitusi wanaeleza lengo la mkutano huo unaowaleta
pamoja washiriki kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi,
Zanzibar na majaji wa mahakama ya rufani ya Afrika Mashariki.
Kwa upande wake mwakilishi wa jaji mkuu wa Tanzania, Mh. Jaji
Edward Lutakangwa amesema kaulimbiu ya mkutano huo ambayo inasema
kuimarisha imani ya wananchi kwa mahakama za Afrika Mashariki kupitia
uwajibikaji na mifumo ya kupima utendaji na usimamizi wa mashauri
inalenga katika kupanua misingi ya haki na usimamizi wa dhana ya
uaminifu na uadilifu katika jamii kupitia idara ya mahakama.
EmoticonEmoticon