WAFANYABIASHARA WILAYANI MOMBA WAPONGEZWA KWA KUWA WAELEWA SUALA LA ULIPAJI KODI SERIKALINI

Na Saimeni Mgalula,Mbeya

Afisa forodha Mfawidhi wa (TRA) Raymond Mwanisawa wa kituo kidogo cha Tunduma kilichopo Wilaya ya Momba,Mkoani hapa,amewapongeza baadhi wa wafanyabashara kwakuanza kuwa waelewa katika swala la ulipaji wa kodi serikalini.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana ofisini kwake,alisema kuwa,walio wengi walikuwa wanakwepakulipa kodi,kwasababu ya kutokujua kwamba ulipaji wa kodi ni wajibu wao,kwani walichokuwa wanajua ni kwamba mapato hayo wanakula viongozi wa TRA,alisema Raymond

‘’alisema  kuwa,lakini kutokana na kutoa elimu kwa wafanya biashara mara kwa mara  kumepelekea baadhi yao kutokuwa wabishi,alitoa mfano kuwa mnakuta mfanyabiashara anakwepa kulipa kodi kumbe bidhaa zake hazitakiwi kulipia kodi alisema alisema Raymond.

Vilevile alifafanua juu ya watu ambao wanakwepa kodi na kupitisha mizigo yao kwa njia za panya bila ya kulipia faini yake kwa gari ni dora Elfu tano (5000) kwa gari bado mzigo ambayo nayo huifanyia Tathimini yake ya kuiripia.

Pia alitoa ushauri kwa wafanyabiasha kwa mwaka huu mpya,alisema kuwa wafanya biashara wafahamu kwamba kulipa kodi ni kwaajili ya umma na pesa hizo hizo ndio zinazotumik a kutengenezea barabara kama barabara ya Mpanda mpaka sumbawanga ni TRA NA Tunduma mpka mpanda ni kwa hisani ya watu wa Marekani alisema Raymond.

‘’Aliendelea kwa kusema kuwa wasibebe didhaa bila kulipia ushuru na alitoa ufafanuzi wa baadhi ya bidhaa ambazo hawalipii ushuru alisema mfano Tackita halina ushuru ila vifaa vyake ndo vinatolewa ushuru alisema hivyo Raymond

N a kwa upande wa baadhi ya wafanya biashara ambao majina yao hawakupenda yaandikwe kwenye gazeti walisema kuwa hata sisi inatakiwa tubadilike ili kuepuka kusumbuliwa na TRA kwani mtu ukilipia mzigo na kibali ukiwa nacho hawatakusumbua waliema wafanya biashara hao .

Pia waliwataka Wafanya biashara wenzao kuwa,wawe wepesi wa kulipa kodi ili kuepuka usumbufu kwasasabu unakwepa alafu,ukija kushikwa unakuja kulipa mara nne yake,sasa hapo unakuwa umefanya nini walisema hivyo.

Na mwisho walimalizia kwa kusema kuwa wafanya biashara tulio wengi hatuja soma kwahiyo wameiomba serikali kutoa elimu zaidi juu ya ulipaji wa kodi kwa wafanya biashara ili wawe na uelewa juu ya maswala hayo na sio kukwepa walimalizia hivyo.

Previous
Next Post »