

Shughuli za mazishi ya mtoto wa miaka miwili zimefanyika nchini Uganda, mtoto ambaye kifo chake kimezua ghadhabu baada ya mtoto huyo kugongwa na gari la halmashauri ya jiji la Kampala ,baada ya mama yake kukamatwa akiuza matunda kinyume cha sheria.
Familia ya Ryan Ssemaganda na wanasiasa wa upinzani walitishia kutomzika mtoto huyo mpaka maofisa hao watakapo wajibika kwa kitendo hicho.Mwili wake ulichukuliwa wakati wakiandamana kuelekea bungeni siku ya alhamisi.
Raia wa Uganda wanaona kuwa halmashauri hiyo inatumia nguvu nyingi kupambana na wachuuzi wa mitaani.
EmoticonEmoticon