KESI YA SHEKH YASOGEZWA MBELE MPKA MEI 14 MWAKA HUU

Katibu  wa Taasisi na Jumuiya ya Waislamu Tanzania , Sheikhe Ponda Issa Ponda ( mwenye kanzu) akisindikizwa na baadhi ya Askari Kanzu na wakawaida


Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mkoa wa Morogoro kwa mara nyingine leo imeshindwa kuanza kusikiliza kesi  ya Katibu wa Taasisi na Jumuiya ya Waislamu  Tanzania , Shehe Ponda Issa Ponda kutokana na  jadala halisi  kutorejeshwa kwenye  Mahakama hiyo toka Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam na  hivyo kuiahirisha hadi Mei 14, mwaka huu.

Katibu  wa Taasisi na Jumuiya ya Waislamu Tanzania , Sheikhe Ponda Issa Ponda ( mwenye kanzu) akiwa ndani ya chumba cha Mahakama akisubiri hatima ya kesi yake 
Katibu  wa Taasisi na Jumuiya ya Waislamu Tanzania , Sheikhe Ponda Issa Ponda ( mwenye kanzu) akisindikizwa na baadhi ya Askari Kanzu na wakawaida , kutoka Mahakamani
Baadhi ya wafuasi wa Katibu  wa Taasisi na Jumuiya ya Waislamu Tanzania , Sheikhe Ponda Issa Ponda wakitoka kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro

Shehe Ponda alifikishwa Mahakamani hapa majira ya saa tatu  asubuhi  chini ya Ulinzi mkali wa Polisi ,ambapo pia baadhi ya wafuasi wake  walifika mapema  Mahakamani hapo  wakitakiwa kubakia nje ya uzio .
Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mkoa  , Mary Moyo , anayesikiliza kesi hiyo alitumia dakika tatu  kufikia kutoa  maamuzi  kuahirisha  kutokana na Jadala halisi la kesi kuendelea kubakia Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Aliufahamisha upande wa wakili wa serikali na Wautetezi  kuwa hakuwa na jalada halisi la kesi hiyo  na  bado haijarejeshewa toka  Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,  lilipopelekwa kwa ajili  ya kusikilizwa ombi la Sheikhe Ponda la mapitio lililowasilishwa kwenye Mahakama kuu hiyo siku za nyuma.
Sheikhe Ponda  amefuguliwa  kesi namba 128/2013 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Morogoro  akikabiliwa na  Mashitaka  matatu ambayo aliyatenda Augosti 10, 2013, eneo la Kiwanja cha Ndege,  Manispaa ya Morogoro na alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza  Augosti 19, 2013.
Previous
Next Post »