Mwanafunzi akatwa Koromeo na kufariki dunia


DSC04900
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tukio la Mwanafunzi kukatwa Koromeo.
Na Nathaniel Limu, Iramba
MWANAFUNZI wa Darasa la kwanza katika shule ya msingi kijiji cha Tatu kata ya Kiomboi tarafa ya Kisiriri wilaya ya Iramba Mkoa wa Singida,Geofrey Emmanuel (9) amefariki dunia baada ya kukatwa koromeo kwa kisu na kusababisha kuvunja damu nyingi.
Inadaiwa kuwa mwanafunzi huyo alichinjwa kinyama na Francis Lukumbitio (30) mkazi wa kijiji cha Kizenga ambaye naye aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kumwagiwa Petroli na kisha kuwashwa moto.
Kamanda wa Mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela amesema tukio hilo la kusikitisha limetokea Desemba 15 mwaka huu saa 10.00 jioni katika kijiji cha Tatu kata ya Kiomboi wilaya ya Iramba.
Amesema siku ya tukio mwanafunzi huyo akiwa anachunga mbuzi pamoja na watoto wenzake ghafla alitokea Francis akiwa amebeba kisu mkononi na kumshika kwa nguvu na kuanza kumkokota hadi kichakani na kisha kutekeleza unyama wake huo.
Akifafanua zaidi, amesema wenzake waliweza kufuatilia na walipofika eneo la tukio walikuta mwanafunzi huyo tayari amekwishafariki dunia kutokana na kukatwa koromeo.
“Watoto hao baada ya kuona tukio hilo, walitoa taarifa kijijini na haraka wananchi waliweza kukusanyika na kumfuata mtuhumiwa kijijini kwake Kizega na walifanikiwa kumkuta Francis akiwa nuyumbani kwake Walimtoa nje na kuanza kumpiga kwa fimbo, marungu na mawe na alipokuwa taabani walimwagia petroli na kumwasha moto”,amesema Kamwela.
Kamanda Kamwela amesema wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na mauaji hayo ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi kuacha mara moja tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake wawafikishe watuhumiwa kwenye vyombo vya dola ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.
Previous
Next Post »