Rais
Jakaya Mrisho Kikwete leo ameongoza maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru
wa Tanganyika uliopatikana Desemba 9, 1961.
Miaka
52 imetimia tangu Tanganyika (sasa Tanzania), kupata uhuru wake kutoka kwa
wakoloni wa Kiingereza, Desemba 9, mwaka 1961.
Maadhimisho
haya yamefanyika uwanja wa uhuru hapa Dar es salaam,Rais Jakaya Kikwete
amekagua gwaride la vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama ambavyo pia vimetoa
heshima kwa kiongozi huyo kwa mwendo wa pole na haraka.kikosi cha anga pia
kimetoa heshima zake na burudani mbalimbali ikiwamo ngoma na michezo
ya halaiki.
Sherehe hizi zimehudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa wa ndani
na nje ya nchi, wakiwamo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.
Katika
maadhimisho haya kwa mwaka jana, yaliyohudhuriwa na viongozi 14 wa kutoka
Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Rais Kikwete
aliwataka Watanzania kujivunia na kuyaenzi mafanikio ya kisiasa, kiuchumi na
kijamii yaliyopatika tangu nchi ilipopata uhuru.
EmoticonEmoticon