WAHUU NA NAMELESS WAPATA MTOTO WA KIKE


Mwisho wa wiki iliyopita umekuwa ni wa kipekee na wa kihistoria kwa Nameless pamoja na Baby Mama wake, Wahu Kagwi baada ya kumkaribisha mtoto mpya katika familia yao, mtoto wa kike ambaye wamempatia jina Nyakio Mathenge.
 
Mtoto huyu anakuwa ni wa pili katika familia hii ya wasanii hawa wanaokubalika sana katika tasnia ya muziki ndani na nje ya Afrika Mashariki, akiwa ametanguliwa na Tumiso ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 8.
 
Wahu ndiye ambaye alikuwa mtu wa kwanza kuwapatia mashabiki na wapenzi wa kazi zao za muziki ambao pia wanafuatilia kwa karibu maisha yao habari za kuzaliwa kwa mtoto huyu, kupitia mtandao wa Facebook, sambamba na kumtakia mume wake maadhimisho mema ya siku yake ya kuzaliwa.
Previous
Next Post »