Vijana watakiwa kuwa na fikra za kimkakati ili kukabiliana na changamoto zinazowakabili katika kupambana na umasikini.

CHIMBO12-12

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akiwasilisha mada kuhusu fikra za kimkakati kwa Vijana jijini Dar es Salaam katika Kongamano la vijana lililoandaliwa wa Kanisa la Nchi ya Ahadi kupitia kituo chake kinachojulikana kwa jina la CHIMBO School of Thought.

Rai hiyo imetolewa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Tanzania kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel alipokuwa akiwasilisha mada juu ya vijana kuwa na fikra za kimkakati katika kongamano lililoandaliwa na Kituo cha Vijana kinachojulika kwa jina la Chimbo School of Thought jijini Dar es Salaam.

Profesa Ole Gabriel amesema kuwa inakuwa ni tatizo kwa vijana kupambana na changamoto za maisha kwa kuwa vijana wengi hawaweki mikakati katika fikra zao.

Aidha  Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa takwimu zinaonyesha takriban asilimia 35.1  ya idadi ya watu ni Vijana na ambapo vijana wanachua karibu asilimia 70 ya nguvu kazi,hivyo wasipo kuwa na fikra na kupanga mambo yao kimkakati nchi itapata hasara.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Chimbo School of Thought Mchungaji Harris Kapiga amesema kuwa kwa kutambua umuhimu wa vijana kama nguvu kazi ya taifa kituo chake kimenuia kubadilisha vijana wengi nchini ili wawe na mitazamo chanya ili wajiletee maendeleo yao wenyewe.

Mchungaji Kapiga amesema kupitia kituo chake vijana wengi wamebadilika kimtazamo na kutoa wito kwa vijana wengi kushiriki katika makongamano mbalimbali yanayoandaliwa kwa ajili yao ili wajifunze na kupata ufahamu wa mambo mengi zaidi.

Previous
Next Post »