DK KIKWETE NA MWENYEJI WAKE BARACK OBAMA MARA BAADA YA KUTUA TANZANIA


Festive: The President was seen dancing along to the music on the red carpet at the airportRais wa Marekani akicheza muziki wa band wakati alipot
ua uwanjani
 Obama akiwa na mwenyeji wake Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Rais wa Marekani Barack Obama amewasili nchini Tanzania leo Jumatatu kwa ziara ya siku mbili, ikiwa ni kituo chake cha mwisho cha ziara yake barani Afrika akitokea nchini Afrika Kusini.
Obama ambaye ameambatana na mkewe Michelle Obama amepokelewa na mwenyeji wake rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Salma Kikwete katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na kisha kuelekea Ikulu ya rais. NA MPEKUZI

Festive: The President was seen dancing along to the music on the red carpet at the airport


Rais Obama na mwenyeji wake wanatarajiwa kufanya mazungumzo ya pamoja na kisha Obama atafanya mazungumzo na waandishi wa habari kabla ya kushiriki dhifa ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali hapo baadaye Ikulu jijini Dar es Salaam.

Aidha hapo kesho Obama atatembelea kituo cha umeme cha Ubungo , baada ya kuahidi kutoa dola za Marekani bilioni saba kusaidia mradi wa umeme Barani Afrika.

Mpango huo wa serikali ya Marekani utazinduliwa kwanza katika nchi za Ethiopia, Ghana, Kenya, Liberia, Nigeria na Tanzania ambazo wananchi wake wanakumbwa na matatizo ya upatikanaji wa umeme.

Welcome: Well-wishers line up in Dar es Salaam in anticipation of Mr Obama's visit
Karibu Barack Obama kanga pamoja na vitenge waliova wananchi wa waTanzania 

Katika ziara yake Barani Afrika iliyoanzia nchini Senegal, Afrika kusini na hatimaye nchini Tanzania Obama amekuwa akisisitiza suala la demokrasia ambapo ameeleza kuwa Afrika itakuwa na mustakabali mzuri kwa kuwa na viongozi wanaopambana kuhakikisha raia wao wanakuwa na maisha bora.

Katika ziara yake nchini Afrika Kusini , Obama hakusita kusifu jitihada za kiongozi wa zamani na baba wa taifa hilo Nelson Mandela ambaye ameeleza kuwa jitihada zake za ukombozi kwa raia wa taifa hilo zilimsukuma kuingia katika siasa na hatimaye kuwa rais wa kwanza mweusi nchini Marekani
Previous
Next Post »