RAIS OBAMA akitelemka kwenye Air Force One na mtoto wake pembeni mara baada ya kuwasili katika ardhi ya Tanzania wakati akitokea afrika ya Kusini majira ya saa 8 mchana kwa ziara ya kikazi nchini.
Barack Obama akipokewa na Wananchi wa  Tanzanian huku wanaband  wakitumbuiza nyimbo mbalimbali kwenye uwanja wa Mwl.Julius Kambarage  jijini Dar es Salaam leo hii mchana akitoka Africa kusini.
Rais Obama akipita kwenye kapeti jekundu huku akiwa na furaha na kucheza nyimbo za wabongo kwenye uwanja wa jijini Dar es salaam wa Mwl. Julius Kambarage mchana wa leo.
Karibu Tanzania....karibu!!!
Ilikuwa ni patashika kwa wacheza ngoma hapa!!! Obama mpaka akaachia Tabasamu
Angalia Rais Obama akicheza nyimbo za hapa kwetu Bongo huku akiwa na furaha kwa mapokezi baada ya kukanyaga ardhi ya Tanzania leo hii mchana kwenye muda wa saa nane na dakika 37.
Rais na First Lady Obama wakisalimia wananchi wa Tanzanian baada ya kupokewa na Rais Jakaya Kikwete na First Lady Salma
Ni furaha hapa baada ya Rais Obama kutua Bongo, hapa anaonekana na mwenyeji wake rais Jakaya Kikwete wakipokewa kwa ngoma
Karibu jamani ....jaribu mzee!!! Tunakupenda!!
Mapokezi haya!!! angalia mavazi!!
Rais Obama atakuwepo hapa nchini kuanzia leo Jumatatu tarehe 1 mpaka tarehe 2 kesho kabla ya kuondoka
Hapa ni wakati wapo Africa kusini wakipanda Air Force One Cape Town wakiwaaga wananchi nchini humo kabla ya kuja Bongo Tanzania leo mchana
Rais Barack Obama wa Marekani (kushoto) akizungumza katika mkutano na  Waandishi wa habari wa Tanzania na Kimataifa Ikulu Jijini Dar es Salaam  jioni hii ambapo mbali na kuzungumzia mstakabali wa ziara yake nchini  Tanzania na Afrika pia amezungumzia masulala mbalimbali ya Kimataifa  ukiwepo mgogoro na Vurugu zinazoendelea nchini Misri na Congo DRC.  Rais George W. Bush na mkewe pia wapo hapa nchini Tanzania na pia watajumuika pamoja na Mr Obama Kesho.
Mr Obama alipotembelea jengo la magereza ambapo Nelson Mandela alifungwa kwa miaka kadhaa huko Africa kusini kwenye kisiwa cha Robben Island.
EmoticonEmoticon