Chris Brown kasema kwa sasa kaamua kuwa single ili kuweka umakini wote kwenye muziki wake

 Chris Brown and His Girlfriend

Miezi kadhaa baada ya kumbwaga Rihanna, mwimbaji Chris Brown aamua kumbwaga girlfriend wake mpya, Karrueche Tran.

Mwimbaji huyo amedai sababu ya kuachana na girlfriend wake huyo mpya ni kwamba kwa sasa anahitaji kuwa single ili kuweka mawazo yake yote kwenye kazi yake ya muziki.

Alipohojiwa na Hollywood Life, Chris Brown alisema;

“Mashabiki zangu wamekuwa wakiniona kwenye mahusiano ya kimapenzi na wasichana tofauti tofauti, mnawajua ni akina nani, lakini kwa sasa mimi kama mwanaume mwenye miaka 24, nimeamua kuwa single.”

“Bado nina urafiki nao mzuri. Kwa sasa nimeamua kuweka umakini wote kwenye muziki wangu kwani niko kwenye kiwango changu cha juu kwa sasa.”

Previous
Next Post »