Wanasayansi waibuka na upandikizaji mpya


Mbinu za kibaolojia zimegundua uumbaji mpya wa binadamu baada ya kuchukua sehemu ya muunganiko wa mbegu ya kiume na yai la mwanamke ‘kiinitete’ hatimaye kuumba mtoto aliyekulia katika maabara.

Wanasayansi wanataja chembe hai hizo kuwa zinajulikana kama ‘Stem Cell’, ambazo hugawanyika na kuzidi kuzaliana. Wanaeleza kwamba chembehai hizo zinaweza kuzalisha binadamu wengine iwapo zitaachwa zizaliane kwa muda mfupi.

Hata hivyo wanabainisha kuwa chembehai hizo zitasaidia pia kutibu magonjwa kama ya kusahau pamoja na magonjwa mengine ya mfumo wa fahamu (Alzheimer desease).

Matokeo ya utafiti huo yanaibua uwezekano wa watoto hao kukulia maabara hali inayoelezwa kwamba itawaruhusu wanandoa wanaoshindwa kupata watoto kwa njia ya kawaida kuunda mtoto kupitia njia hii.

Ingawa tangu awali kiinitete cha binadamu kilikuwa kikipandikizwa, lakini hivi sasa kumekuwa na uwezekano wa kuchukua chanzo cha chembehai nyingine na kuunda mtoto mwingine. Timu hiyo ya wanasayansi kutoka nchini Marekani ilianza kwa kufanya utafiti wa dawa ya magonjwa ya kusahau na mengine ya mfumo wa fahamu, lakini ndani ya utafiti wao ndipo wakagundua kuwa chembehai hizo pia zinaweza kugemwa na kufanya upandikizaji wa mtoto.
Uwezo wa kuzalisha watoto

Mwanzilishi wa timu hiyo ya Human Genetics Alert Dk David King, anasema kuwa duania awali ilifanikiwa kupandikiza mbegu ya kiume na yai la kike, lakini kwa sasa ndani ya kiinitete hicho panaweza kuzalishwa watoto wengi watakaotoka katika mfumo huo.

Awali, mmoja wa watafiti hao Dk Shoukhrat Mitalipov alichukua mayai kutoka kwa mwanamke wa umri wa miaka 27 na kuondoa DNA, kisha baadaye aliweka mbegu za kiume na kukiacha kiini tete hicho kwa kuweka joto la umeme kwa muda wa siku sita, ambapo baada ya kiinitete hicho kutimiza siku sita alifanikiwa kuvuna chembehai hizo kutoka katika kiinitete.

Seli hizo zinazojulikana kama ‘master cells’ zina uwezo wa kugeuka katika kila aina ya seli kwenye mwili, zinaweza kutumika kama dawa maalumu ya kutibu magonjwa kadhaa mwilini na kuponya baadhi ya viungo katika mwili.

Dk Mitalipov aliyetumia miaka mingi katika kufikia mbinu hii anasema; “ugunduzi wa utafiti huu mpya wa kuzalisha seli zinazoweza kutibu magonjwa ya mfumo wa fahamu na ubongo, pia utasaidia kuunda watoto kwa njia ya upandikizaji. Chembehai nyingine zinaweza kutengeneza dawa maalumu ya kutibu magonjwa yanayoathiri mamilioni ya watu duniani, ambayo tutayaweka hadharani baada utafiti zaidi kukamilika.”

“Bado kuna kazi kubwa ya kufanyika ili kuendeleza usalama na ufanisi wa matibabu ya chembehai hii, tunaamini hii ni hatua muhimu katika kuendeleza chembehai zinazoweza kutumika kama dawa,” anaongeza Dk Mitalipov.

Anafafanua: “Matumizi ya yai na mbegu kutoka kwa watu wenye afya yalihakikishwa kuwa yana uwiano katika miili yao, hivyo ndivyo tulivyoweza kupata mafanikio na kuondoa haja ya dawa zenye nguvu kumkandamiza mgonjwa kwa mfumo wa kinga.

source:Mwananchi
Previous
Next Post »