Mtoto aliyetumbukia chooni nchini China arejeshwa kwa mamake.

This frame grab taken from AFPTV footage received on May 28, 2013 shows rescue workers breaking away bits of a pipe to remove a newborn baby boy stuck inside in the city of Jinhua, in the eastern province of Zhejiang.  The newborn baby boy was rescued from a sewage pipe in a Chinese apartment building after being flushed down a toilet, state media said, provoking online outrage on May 28.    CHINA OUT   AFP PHOTO / AFPTV        (Photo credit should read AFPTV/AFP/Getty Images)

Waokoaji wakivunja bomba la maji taka kumuokoa kichanga huyo.

Mtoto mchanga aliyeokolewa kutoka bomba la kupitishia maji taka nchini China amerejeshwa kwa mama yake baada ya maafisa wa polisi kubaini kuwa kutumbukia  kwake katika bomba hilo ilikuwa bahati mbaya.

Tukio hilo la kuokolewa kwa mtoto mchanga katika jimbo la Pujiang  lilizua shutuma kali kutoka kwa raia wa China na wahisani wengi walijitokeza kumsaidia mtoto huyo wa kiume.

Mtoto huyo tayari amechukuliwa na mama yake kutoka hospitali.

Mwanaume mmoja ameomba uchunguzi wa kubaini kama mtoto huyo ni wake na kusema ikibainika ni hivyo, yuko tayari kujadiliana na mama huyo jinsi ya kumlea.

Polisi wameamua kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 22 hatakabiliwa na mashitaka yoyote.

article-2331941-1A0AF3D2000005DC-345_634x425

 

Mtoto aliyeokolewa kutoka kwenye bomba la kupitisha maji taka baada ya kupatiwa huduma ya kwanza.

Previous
Next Post »