Watano wauwawa katika mapigano Yemen

 
Kiasi watu watano wameuwawa nchini Yemen katika mapigano karibu na eneo lililopita bomba la mafuta mashariki mwa mji mkuu Sana'a.

Mabomba ya mafuta na gesi nchini Yemen yamekuwa mara kwa mara yakihujumiwa na wapiganaji wa Kiislamu ama watu wa makabila tangu kuzuka kwa vuguvugu la maandamano ya kutaka mageuzi na kuharibu kilometa 300 za bomba ambalo linasafirisha mafuta kwenda katika kituo katika bahari ya Sham.

Yemen ni nchi jirani ya Saudi Arabia upande wa kusini na ni mahali ambako kuna tawi linaloendeleza mapambano la al-Qaeda.
Previous
Next Post »