Mwanamke anayetuhumiwa kumtesa kumlisha kinyesi na kumchoma moto mtoto wa kaka yake kumfungia ndani, amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika mahakama ya Wilaya ya Mbeya kujibu shtaka linalomkabili.

 

Mtuhumiwa Wilvina Mkandala (24)
Hataki kabisa kuonyesha sura yake

Aneth akiwa na wazazi wake mahakamani jana
Akirudishwa tena rumande mpaka tena tarehe 27/11

Baadhi ya akina mama wakiwa nje ya mahamaka wakisubiria kumwona mama huyo mwenye roho mbaya
Akina mama hao wakiwa na hasira kali walisikika wakisema tuachieni kidogo tumfunze adabu

MWANAMKE
anayetuhumiwa kumtesa kumlisha kinyesi na kumchoma moto mtoto wa kaka yake kumfungia ndani, amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika mahakama ya Wilaya ya Mbeya kujibu
shtaka linalomkabili.

Mwendesha
mashtaka wa Serikali, Achiles Mulisa ameileza Mahakama kuwa Mtuhumiwa Wilvina Mkandala (24)
Mkazi wa Majengo jijini humo alitenda kosa la kusababisha majeraha akiwa
na nia ovu ambayo imemsababishia ulemavu mtoto Aneth Gasto (4).

Mulisa
akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo Gilbert
Ndeuruo amesema kosa hilo ni kinyume cha kanuni ya adhabu kifungu cha
222(a) sura ya 16 kama ilivyorejewa mwaka 2002.

Kutokana na hali hiyo
mwendasha mashitaka huyo ameileza mahakama kuwa kesi inayo mkabili mwanamke
huyo ilihitaji mashahidi sita ambao ni Dactari aliye mfanyia upasuaji mtoto
huyo mwenyekiti wa Mtaa na barozi wake pamoja na Askari
mpelelezi wa kesi hiyo na mtoto mwenye .

Amesema
teyari mashahidi wanne kati ya sita wamekwisha toa ushahidi wao mahakani hapo .

Kutokana
na kosa hilo mshtakiwa amekana shitaka hilo ambapo alirudishwa mahabusu hadi
Novemba 27 Mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.


Amesema
upande wa Jamhuri unamashahidi wanne ambao watatu kati yao teyari wamekwsha toa
ushahidi wao katika mahakama hiyo .

Amewataja
mashahidi hao kuwa ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Shuku Mwakanyamale, Daktari
anayemtibu mhanga katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya Dr. Paul Kasubi na Habiba Mwakanyamale .


Wengine
ni Askari Polisi aliyepeleza kesi hiyo WP Pudensia na Mtoto mwenyewe ambao wako tayari kufika mahakamani na kutoa
ushahidi wao mbele ya mahakama.


Awali
mshatakiwqa huyo aliieleza mahakama kuwa na uhusiano na mtoto huyo ambapo
pia alikiri kuwa na taarifa za kile kinachoendelea juu ya matibabu ya mtoto huyo
na kuhusu kukatwa kwa mkono wake wa kushoto na kufungwa bandeji ngumu(POP)
kwenye mkono uliobaki.
Previous
Next Post »