Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe
 Mosi Mei, 2017 amesema Serikali ya  Awamu ya tano imepanga kufanya  
nyongeza ya kawaida ya kila mwaka katika mishahara yaani Annual 
increment, ambayo ilikuwa imesimama kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na 
promosheni.
Rais
 Magufuli ametoa ahadi hiyo katika Sherehe za siku ya Wafanyakazi 
duniani zilizofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi mkoani 
Kilimanjaro.
Amesema
 uamuzi wa Serikali wa kuanza kutoa promosheni unatokana na kukamilika 
kwa zoezi la uhakiki wa Wafanyakazi hewa  zaidi ya wafanyakzi kumi 
19,000 walibainika kuwa wafanyakazi  hewa.
''Yale
 mambo yote yaliyokuwa pending ikiwa ni pamoja na promosheni kwa sababu 
tulishindwa,  unaweza kupromoti mfanyakazi hewa hayupo,kwa sababu 
tungetoa promosheni wakati kuna wafanyakazi 19,000 hewa,maanake 
tungepromoti na 19,000 na siajabu na watu waliowaandika mule ndio 
wangeletwa katika mapendkezo ya promosheni'' amesema Rais Magufuli.
Aidha,
 Rais Magufuli amewaonya watumishi ambao wamekuwa wakidanganya umri wa 
kustaafu ili waendelee kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwa siku zao sasa
 zimekwisha.
Katika
 hatua nyingine Rais Magufuli amepiga marufuku uhamisho wa Wafanyakazi 
bila kuwalipa stahili zao kutokana na kuwepo na tabia ya kuwahamisha 
wafanyakazi bila kuzingatia taratibu hasa za malipo ya uhamisho.
''Sasa
 niwaombe wafanyakazi yeyote akihamishwa hakuna kuhama mpaka umelipwa 
pesa ya uhamisho,kuanzia juu mpaka chini,yeyote atakaye kuhamisha 
mwambie nipe hela yangu ya uhamisho ninapoenda akishindwa usihame kaa 
hapohapo ufanye kazi'' Amesema Rais Magufuli.
Amesema
 viongozi wengine wamekuwa wakiwahamisha wafanyakazi  kwa maslahi 
binafsi au visasi kutokana na maendeleo wanayowapata wafanyakzi
Rais
 Mgufuli amewahakikishia wafanyakazi kuwa Serikali ya awamu ya Tano 
itaendelea kuwajali na kuwa  karibu nao katika kutimiza dhana ya utatu 
ya ushirikiano kati ya Serikali, Wafanyakazi na Waajiri kwa lengo la 
kuleta maendeleo.
Aidha,
 Rais Magufuli amewaeleza wafanyakazi mipango mbalimbali anayofanywa na 
Serikali katika kuwaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na ununuzi wa ndege 
mpya ,ujenzi wa Reli ya kisasa, utoaji elimu bila malipo na uboreshaji 
wa miundombinu katika kuwaletea maendeleo wananchi.
Sherehe
 za Mei Mosi zilizofanyika katika mkoa wa Kilimanjaro pia zimehudhuriwa 
na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim 
Majaliwa, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, 
Wabunge na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali ambapo kauli mbiu 
inasema,'' Uchumi wa Viwanda uzingatie kulinda Haki, Maslahi na Heshima 
ya Mfanyakazi''.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Moshi, Kilimanjaro
1 Mei, 2017
 
 

EmoticonEmoticon