HAYA NDIO MAMBO AMBAYO UBONGO WA KIJANA UNATAKIWA ULISHWE NA SIO KUDANGANYWA TU MAENDELEO NA NYIE MNAKUBALI TU BILA KUJUA HAYO MAENDELEO TUNAYAFIKIAJE ASANTE mrproblemsolved Na IMANI KAJULA KWA KUTUKUMBUSHA VIJANA NINI TUNATAKIWA KUFANYA.



Hivi una habari kwamba usipojua kuchagua utajiri kila siku utachaguliwa na umaskini kila siku?

Vijana tunakula njaa ya nguvu miaka mingi kwasababu ya matatizo mawili.

1) hatujui kutambua fursa zikiwa mbele yetu kwasababu tuko bize kutafuta MTU wa kutusaidia badala ya MBINU ya kutusaidia.

2) tukishapata fursa ya kutoka kimaisha, tunaichukulia poa badala ya kuikumbatia kama vile ni pumzi yetu ya mwisho, na kuchukua hatua zote za kuhakikisha haipotei kabla haijazaa matunda.

Wewe ambae bado unasota kila siku kutafuta maisha, umejiuliza ni wapi unakosea? Safari yako ina ramani yoyote au unaenda tu ilimradi uwe unatembea?

Kwenye mkesha wa leo, chukua hatua ya kutafuta MBINU ya kukufikisha unapotaka kwenda.

Na hatua hiyo ni kujibu kwanza swali lifuatalo: nikiwa nimefikia malengo yangu, maisha yangu yatakuaje kuanzia niamke asubuhi hadi nilale jioni? Simulia maisha hayo.

 


Matarajio yanayojengwa kwa wapiga kura Vijana ni makubwa MNO. Ukweli utabaki hakuna Chama wala Serikali itakayoleta maendeleo mlangoni. Ni kwa jitihada na kazi.
Previous
Next Post »