Kiwango cha ufaulu mtihani wa kidato cha pili cha ongezeka kwa asilimia 92 mwaka 2014.


Baraza la mitihani la tanzania limetangaza matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha pili kwa mwaka 2014 huku kiwango cha ufaulu kikiongezeka kutoka asilima 89 hadi asilima 92 kwa mwaka 2014 ikiwa ni ongezeko la asilimia 3.
Pamoja na kupanda kwa ufaulu wa jumla  takwimu zinaonesha kuwa ufaulu wa masomo ya sayansi yakiwemo hisabati na biashara upo chini ya asilima hamsini hivyo juhudi za makusudi zinahitajika kuendelea kufanyika ili kuinua kiwango cha ufaulu wa masomo hayo.
 
Kutokana na matokeo hayo walimu na wafunzi wametakiwa kuendeleza juhudi katika ufundishaji na ujifunzaji katika masomo ambayo wanafunzi wameonekana kutofanya vizuri waongeze juhudi kwa kipindi kijacho  waweze kufanya vyema.
Previous
Next Post »