WANANCHI WA MITAA YA CHIPAKA NA NDELEMA KATIKA MJI MDOGO WA TUNDUMA WAKERWA NA TANIA YA UTORO WA WAALIMU.

Na Lupakisyo Kingdom ,Momba –Mbeya.

WANANCHI katika mitaa ya  Chipaka , Ndelema katika mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya wamekerwa na na vitendo vya baadhi ya walimu katika shule ya msingi Chipaka   kuwa watoro na kurudisha nyuma mapango wa serikali katika kutekeleza mpango wa matokeo makubwa sasa  katika wizara ya Elimu.

Hayo yamesemwa na baadhi ya wananchi wa katika mitaa hiyo walipokuwa wakizungumza  na  mwandishi wetu  jana , walisema kuwa kuna baadhi ya walimu wanaingia shuleni muda wa saa tatu na ifikapo saa  sita wanapanada magari na kuludi makwao ambapo ni nje ya utalatibu wa kazi yao.

‘’Tunajua kuwa sheria na utalatibu wa shule zote za msingi Nchini ni kwamba walimu muda wa kuingia shuleni ni saa mbili asubuhu na muda wa kutoka ni saa kumi jioni nje na hapo kama kuna dhallula lakini kwetu yamekuwa kama maoea’’ alisema kijana mmoja ambaye hakutaja jina.

Walisema kuwa wanafunzi muda wa saa sita baada ya kuondoka kwa walimu baadhi na kubaki baadhi  yao ambao wanafuata sheria za ajira yao  nao wanafunzi  wanaamua  kuludia makwao maana wanabaki wanacheza bila kufundishwa.

‘’Endapo wataendelea bila ya kuchukuliwa hatua basi mpango wa serikali ya jamhuli ya muungano wa Tanzania wa matokeo makubwa sasa katika wizara ya elimu tusahau na itabaki kuwa kauli mbiu isiyo kuwa na utekezaji’’ ,walisema.

Walisema kuwa inaonekana kwa upande ya uondozi wa wilaya wanaonekana wameshindwa kulitatua hili hivyo tuanamuomba waziri mwenye dhamana Shukulu Kawmbwa asikie kilio cetu maana hasala ni kwa watoto wetu ambao wanaishia kuolewa.

Walisema kuwa kuna baadhi ya walimu tumewahi kuwahoji na walicho chibu ni kwamba badhi hawawezi  kuwajibishwa maana ni marafiki na badhi ya wafanyakazi katika ofisi za wiraya katika wizara ya Elimu.

‘’Usistajabu kuona baadhi yao unawakuta katika shughuli binafsi muda ambao walistahili kuwa dalasani kuwafundisha watoto wetu  ambapo wanajivunia kuwa wamesoma na maofisa elimu’’ walisema kwa uchungu.

Aidha baadhi ya wanafunzi walisema kuwa hiyo inasababisha saana kupolomoka kwa elimu katika shule hiyo ambapo kwa mwa huu walio hitimu shule ya msingi walikuwa wanafunzi 28 na walio faulu kujiunga na masomo ya shule ya Upili ni wanafunzi saba tu.

Akizungumza kwa siri kubwa mmoja wa walimu shuleni hapo alisema kuwa inaonesha shule hiyo baadhi ya walimu wanathamini saana kazi binafi kuliko shughili rasimi na wanayo itegemea kuendeshea maisha.

‘’Kuna baadhi ya walimu hawaonekani kazini wiki nzima na bila ya mkuu wa shule kujua waliko hii inatuathili saana kuendelza shule yetu ambapo muda mwingine wanashindwa kumaliza maada zote na inatubidi tuwasaidie kufundisha ili kuenda nao sambamba’’ alisema.

‘’Hohao ndio wamekuwa kipau mbele katika migomo pindi serikali ikwamapo kutoa masirahi yetu kwa  wakati bila ya kujijaji wao wenyewe tabia walio nayo ya kutofuata taratibu za shule’’ Aliongeza.

Akijibu kilio hicho cha wazazi mwalimu mkuu wa shule hiyo Mwampashi  Araija kwa njia ya simu alisema kuwa yeye ni mgeni na shule hiyo nab ado hajaanza kufanya kazi.

Alisema kuwa wanachosema wananchi huenda ni kweli maana hawawezi kuongea kitu kisicho kuwepo na kuamua kumsingizia walimu.


‘’Ndio mimi nimeshalipoti shuleni hapo ila nilipoti mwishoni mwa muhula wa mwisho na nalijitambulisha  kwa walimu wote ila kujua mwenendo wa mwalimu mmoja mmoja sijajua na kuna baadhi ya walimu siku ya kulipoti hawakuwepo niliwakuta wachachae’’ alisema Mwampashi.

‘’Kama kuna matatizo ya aina hiyo naahidi kuya maliza maana tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria bila kufuata sheria zinazo kuongozo hufai kuitwa mwalimu ‘’ alisema mwampashi.

                                                    
Previous
Next Post »