Asilimia 52 ya Watanzania wanawake kwa wanaume imedaiwa kuwa wanatumia vipodozi ambavyo si salama kwa afya zao na ambavyo matumizi yake yamepigwa marufuku nchini.
Baadhi ya vipodozi vilivyopigwa marufuku kutokana na kusababisha madhara ya kiafya.
Afisa kutoka asasi ya Envirocare Bi. Ephrasia Shayo amesema hayo leo wakati wa kampeni ya kuzuia matumizi ya vipodozi hatari inayoendeshwa na asasi hiyo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA.
Bi. Ephrasia ametaja baadhi ya madhara yanayotokana na matumizi ya vipodozi hivyo kuwa ni saratanio ya ngozi, kuzaa watoto wenye ulemavu wa akili, kuharibika kwa mimba, maelezo ambayo yameungwa mkono na muelimishaji umma wa TFDA Bw. James Ndege.
Kwa mujibu wa Ndege, idadi kubwa ya vipodozi hivyo imeingia nchini kwa njia za panya kutokana na hatua zinazochukuliwa na TFDA kudhibiti uingiaji wa vipodozi hivyo katika mipaka.
Amesema watu wengi wanakimbilia kunua vipodozi hivyo kutokana na kuuzwa kwa bei nafuu ambayo kila mwananchi anaweza kuimudu pasipo kujali madhara anayoweza kuyapata.
Muelimishaji huyo kutoka TFDA amewataka wananchi kuchukua tahadhari zote kuepuka matumizi ya vipodozi hatari, kama vile vyenye madini ya zebaki, hydroquinone na nyinginezo ambazo zikiingia mwililini zinaleta madhara makubwa kwenye viungo vya ndani ya mwili.
Artikel Menarik Lainnya
Rais Magufuli Asema Hatagawa Chakula cha Bure Kwa Watakaopatwa na Janga la Njaa Bila Sababu za Msingi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali
Mbowe Ahojiwa na Kuachiwa Kwa Dhamana.......Tundu Lissu Asisitiza Oparesheni UKUTA Iko Palepale MWANASHERIA Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Li
Rais Dkt. Magufuli aahidi neema kwa wafanyakazi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, l
Wagonjwa wa Saratani Ocean Road kunufaika na huduma za TEKNOHAMA Vodacom Tanzania Foundation yatoa msaada kufanikisha mchakato huo Wahanga w
TRA Yaja na Mikakati 5 Ukusanyaji Kodi. MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka mikakati mitano ya kuboresha ukusanyaji kodi ya
More 1 of 376 TAASISI YA KILIMANJARO DIALOGUE YATAKA WANAHABARI KUTUMIA KALAMU ZAO KUDUMISHA AMANI NCHINI Mdhamini wa Taasisi ya Kilimanjaro Dialogue, Habib Miradji (katikati) akiongoza m
EmoticonEmoticon