Walimu shule ya msingi Endeshi karatu,wakimbia na kubaki mwalimu mmoja tu.

Walimu  wote  waliopelekwa na  serikali katika  shule ya msingi ya  Endeshi iliyoko kijiji cha matala kata ya barai wilayani Karatu mkoani  Arusha wameacha kazi na kutorokea kusikojulikana na kumuacha  mkuu wa shule peke yake kwa kile kilichodaiwa kuwa ni mazingira magumu ya eneo hilo.
Mkuu wa shule hiyo  Bw Pilemon Amsi  amesema tatizo kubwa  ni  kukosekana kwa mahitaji muhimu zikiwemo nyumba za walimu  na  kwamba amebaki peke yake hali inayomfanya ashindwe kutoa  huduma  ,na hali inaendelea kuwa mbaya kwani wanafunzi nao wanaendelea  kutoroka.
 
Afisa mtendaaji wa  kijiji hicho Bw, Gitoyanga Gweku amesema  pamoja na tatizo la ugumu wa mazingira walimu wanaopelekwa  kwenye shule hiyo ni wale waliokata tamaa  na  walioshindikana kwenye maeneo mengine.
 
Nao badhi  ya wazazi  wamesema hawaoni sababu ya kuwalazimisha  watoto wao kwenda shule ambayo haina walimu kwani ni kupoteza  muda na kwamba ni bora wafanye kazi zingine ikiwemo ya kuchunga mifugo.
 
Mkuu  wa  wilaya  ya  karatu Bw Felexs Ntebenda ametembelea shule  hiyo na kujionea hali  halisi  na amesema serikali itawatafuta  walimu  waliotoroka popote walipo kwani  hata  kama kulikuwa na tatizo  ufumbuzi wake sio kutoroka  na kuwatelekeza wanafunzi.
Previous
Next Post »