Serikari yatakiwa kuchukua hatua kudhibiti ugonjwa wa ebola mipakani

Wakati watu zaidi ya 1,000  wanaripotiwa kufa kutokana na ugonjwa wa Ebola katika nchi za afrika magharibi, hadi sasa serikali kupitia wizara ya afya na usatawi wa jamii haijachukua hatua zozote za tahadhali hasa kwa kutoa vifaa vya kujikinga na kutambua dalili za ugonjwa huo katika mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari.
Uchunguzi  katika mpaka huo wa Sirari ambao unatumika  kuingiza wageni kutoka nchi mbalimbali kupitia nchini Kenya na Uganda umebaini kuwa tangu  kuibuka kwa ugonjwa huo mwezi mmoja ulipita  katika nchi za afrika magharibi, serikali  haikuchukua tahadhali yoyote  ya kujihami na ugonjwa huo kwa  kushindwa ya  kusambaza vifaa  vya  utambuzi wa ugonjwa Ebola hatua ambayo imefanya wageni kuingia nchini bila ya kuchunguzwa.
 
Afisa afya mfawidhi kituo cha afya bandari ya Sirari Bw Salvatory  Ludovick, amesema kutokana na ukosefu wa vifaa  vya kutambua  ugonjwa huo, hivi  sasa  wanalazimika kuwakagua  wageni  kwa hisia  hasa kulingana na mataifa  wanayotoka  pamoja na  kuchukua taarifa  zao muhimu.
 
Naye mganga mkuu wilaya ya Tarime Dk Charles Samson wa  mjini Tarime amesema wilaya imechukua hatua za kutoa matangaza katika vituo  vya afya  kuzunguka mpaka wa  Sirari wakati  wakingojea msaada  wa  vifaa  vya kinga na utambuzi wa ugonjwa huo  kutoka wizara ya afya na ustawi wa jamii, huku  baadhi ya  wananchi katika mpaka wa Sirari wakiitaka serikali kuchukua hatua za haraka za  kujihami na ugonjwa huo hatari.  
Previous
Next Post »