Kaimu
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya,
BARAKAEL .N. MASAKI – ACP anawatangazia Wananchi wote ya kuwa orodha ya
majina ya vijana waliomaliza Kidato cha Nne mwaka 2013 na cha Sita mwaka 2014
na kuchaguliwa kufanya usalii wa kujiunga na Jeshi la Polisi inapatikana kwenye
tovuti ya Polisi: www.policeforce.go.tz au wafike ofisi ya
kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya iliyopo Forest jirani na Mahakama kuangalia majina yao.
Muhimu:
·
Mwombaji anaruhusiwa
kufanya usaili kwenye kituo chochote cha usaili kilicho karibu naye kulingana
na tarehe zinavyoonesha kwenye jedwali hapo juu ili mradi tu awe
amejiridhisha kuwa ni miongoni mwa walioitwa kwenye usaili. Jeshi la Polisi
halitahusika na lawama yoyote ile kwa mtu atakayekwenda kwenye kituo cha usaili
hali ambapo jina lake si miongoni mwa walioitwa kufanya usaili.
·
Mwombaji aliyeitwa
kwenye usaili aje na vyeti vyake vyote vya masomo [(Academic
Certificate(s)/Results slip(s) & Leaving certificate(s)], nakala halisi ya
cheti cha kuzaliwa (Original Birth certificate). Hati ya kiapo cha kuzaliwa
haitakubalika.
·
Mwombaji awe na
namba ya simu itakayotumika kumjulisha endapo atachaguliwa..
·
Kila mwombaji
aliyeitwa kwenye usaili atajigharamia usafiri, chakula na malazi kwa muda wote
wa zoezi la usaili. Pia waombaji waje na kalamu za wino kwa ajili ya usaili wa
kuandika.
Ni muhimu sana kwa kila mwombaji kuzingatia
muda wa kuanza usaili.
TAREHE YA USAILI KWA MKOA WA MBEYA NI 28.09.2014 HADI 01.10.2014. SAA 08:00 ASUBUHI HADI 10:00 JIONI.
TAREHE YA USAILI KWA MKOA WA MBEYA NI 28.09.2014 HADI 01.10.2014. SAA 08:00 ASUBUHI HADI 10:00 JIONI.
EmoticonEmoticon