Katika mwaka wa fedha
2014/2015 Jeshi la Polisi Tanzania linatarajia kuajiri wahitimu wa vyuo vya
Elimu ya Juu wa mwaka 2013/2014. Ili kutekeleza azma hii waombaji watajaza
kikamilifu na wataambatanisha vivuli vya vyeti vyao na kutuma Makao Makuu ya
Polisi kwa njia ya Posta kabla ya tarehe 31.08.2014 kwa anuani ifuatayo:
Inspekta Jenerali wa
Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
S. L. P. 9141,
DAR ES SALAAM
Makao Makuu ya Polisi,
S. L. P. 9141,
DAR ES SALAAM
WAOMBAJI WAWE NA
TAALUMA ZIFUATAZO:
Shahada: Menejimenti ya Rasilimali Watu, Utawala
katika Utumishi wa Umma, Uchumi, Saikolojia na Ushauri Nasihi, Usimamizi wa
Sheria na Utekelezaji[BaLE], Sheria, Ualimu, Maendeleo ya Jamii, Uandishi wa
Habari, Uandishi wa Habari za Michezo, Mawasiliano ya Umma, TV & Redio
Production, Michezo, Ugavi[BA in Procurement & Supplies], Mawasiliano ya
Redio[Bsc in Radio Communication], Mazingira[BA in Environmental Disaster Mgt],
Uhandisi Mitambo, Uhandisi Madini[Mining Engineering], Uchoraji[BA in Fine
Arts], Fedha na Benki[Finance & Banking], Daktari[Medical Doctor] na
Daktari wa Meno[Dental Surgeon], Mkemia, Bailojia[Molecular Biology].
Stashahada: Utunzaji Kumbukumbu, Katibu
Muhutasi[Personal Secretaries], Mawasiliano ya Redio, Matengenezo ya Kompyuta,
Fax na Photocopy Machines, Mafundi Mitambo wa Meli, Mafundi Umeme wa Magari,
Ugavi[Procurement & Supplies], TV na Video Production, Manahodha,
Tabibu[Clinical Officer], Tabibu wa Meno[Dental Therapist], Mzoeza
Viungo[Psysiotherapist/Occupational Therapist], Fundi Sanifu
Mionzi[Radiographer] na Fundi Sanifu Macho[Optometrist].
Astashahada: Uzamiaji, Mpishi, Fundi Pikipiki, Fundi
Ushonaji na Muuguzi Msaidizi[Enrolled Nurse].
MASHARTI KWA MWOMBAJI
1. Mwombaji atajaza fomu ya maombi kikamilifu na atabandika
picha yake “Ppt Size” kwenye fomu.
2. Mwombaji aambatanishe katika fomu vivuli vya vyeti vyote
yaani cheti cha kuzaliwa, kuhitimu elimu ya sekondari[Leaving
& Academic], cheti/vyeti vya taaluma[Academic Transcript].
3. Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
1. Mwombaji atajaza fomu ya maombi kikamilifu na atabandika
picha yake “Ppt Size” kwenye fomu.
2. Mwombaji aambatanishe katika fomu vivuli vya vyeti vyote
yaani cheti cha kuzaliwa, kuhitimu elimu ya sekondari[Leaving
& Academic], cheti/vyeti vya taaluma[Academic Transcript].
3. Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
SIFA ZA MWOMBAJI
1. Awe Mtanzania kwa kuzaliwa.
2. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 25.
3. Awe amehitimu chuo mwaka wa masomo 2013/2014 tu.
4. Awe na tabia njema.
5. Asiwe na kumbukumbu za kutenda uhalifu.
6. Awe na afya njema[kimwili na kiakili]
7. Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto.
8. Asiwe na alama za kuchora mwilini[tatuu].
9. Awe na urefu usiopungua sentimita 155.
10. Asiwe mtumiaji wa madawa ya kulevya.
11. Awe hajaajiriwa na idara nyingine Serikalini.
12. Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya awali ya Polisi.
13. Awe tayari kufanya kazi popote ndani na nje ya Tanzania.
1. Awe Mtanzania kwa kuzaliwa.
2. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 25.
3. Awe amehitimu chuo mwaka wa masomo 2013/2014 tu.
4. Awe na tabia njema.
5. Asiwe na kumbukumbu za kutenda uhalifu.
6. Awe na afya njema[kimwili na kiakili]
7. Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto.
8. Asiwe na alama za kuchora mwilini[tatuu].
9. Awe na urefu usiopungua sentimita 155.
10. Asiwe mtumiaji wa madawa ya kulevya.
11. Awe hajaajiriwa na idara nyingine Serikalini.
12. Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya awali ya Polisi.
13. Awe tayari kufanya kazi popote ndani na nje ya Tanzania.
Fomu:- Fomu ya Ajira Elimu ya Juu 2013/2014 zinapatikana kwenye tovuti www.policeforce.go.tz au kwa wakazi wa Mbeya wafike ofisi ya
kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya.
EmoticonEmoticon