WAUMINI 30 WA KANISA LA MORAVIAN WAFIKISHWA MAHAKAMANI


WAUMINI wapatao 30 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni leo jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya fujo hadharani katika Kanisa la Moravian lililopo Mwananyamala-Msisiri ” A” Wilaya ya Kionondoni.Katika kesi hiyo iliyounguruma kwa muda wa saa mbilli imeelezwa kuwa Julai 20 mwaka  huu katika  kanisa hilo lililopo eneo la Mwananyamala Msisiri ‘A’ waumini  hao kwa  pamoja walifanya  fujo  zilizosababisha kuhatarisha amani.

Kesi hiyo iliyosomwa na mwendesha mashitaka wa serikali, Credo Rugajo mbele hakimu mwandamizi  wa  mahakama hiyo Boniphace Lihamwike, ilidaiwa kuwa Julai 20 waumini walianzisha mzozo uliosababisha waumini kupigana  na kusababaisha askari  polisi  kutumia  nguvu  kubwa  kutuliza  fujo  hizo  ikiwa ni pamoja na kutumia mabomu ya machozi.

Baada ya  kusikiliza kesi pande zote  mbili, Hakimu Lihamwike alisema dhamana iko wazi  kwa  kila  mtuhumiwa kuwa na mdhamini mmoja anayeaminika na shilingi  milioni moja  kimaandishi kwa  kila  mmoja.
Previous
Next Post »