TANGAZO KUHUSU MV. KIGAMBONI


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UJENZI
WAKALA WA UFUNDI NA UMEME (TEMESA)
temesa
Telegrams TEMESA DSM S.L.P 70704
Simu: +255-22-2862796/97 DAR ES SALAAM
Fax: +255-22-2865835 TANZANIA
________________________________________
TAARIFA KWA UMMA
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) anawatangazia wananchi wote kuwa kivuko cha MV. Kigamboni kinatarajiwa kwenda kwenye matengenezo makubwa wakati wowote kuanzia leo.
Hivyo huduma za uvushaji zitaendelea kwa kutumia vivuko vya MV. Magogoni pamoja na MV. Lami katika kipindi chote cha matengenezo husika.
Uongozi wa TEMESA unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakao jitokeza.
Imetolewa na Ofisi ya Mtendaji Mkuu 
TEMESA
23/7/2014
Previous
Next Post »