Abiria kadhaa waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya japanese aina ya Yutong kutoka Ikonda wilayani Makete kwenda Makambako, wamenusurika kifo huku wengine wakijeruhiwa baada ya basi hilo kutumbukia mtoni.
Ajali hiyo mbaya imetokea kwenye daraja lililopo eneo la Mpandu wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe jana majira ya saa 9 mchana.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wamedai kuwa imesababishwa na basi hilo lenye namba za usajili T 261 CMK kushindwa kupanda mlima kulikosababishwa na gia kufeli hali iliyopelekea basi hilo kuanza kurudi nyuma kwa kasi hadi kutumbukia mtoni.
Kufuatia ajali hiyo baadhi ya magari yaliyokuwa yakipita eneo hilo yalikuwa yakitoa msaada kwa manusura wa ajali hiyo huku majeruhi wakikimbizwa hospitali ya Kibena mkoani Njombe kwa ajili ya matibabu.
Sista wa kanisa katoliki akiendelea kuugulia maumivu baada ya kunusurika kwenye ajali hiyo
Mashuhuda wa ajali hiyo
Abiria wakipanda basi jingine ili waendelee na safari
Mwandishi wa eddy Blog aliyefika eneo la tukio ameshuhudia baadhi ya abiria walionusurika wakipanda kwenye basi lingine la kampuni hiyo ili kuendelea na safari.
Mmoja wa abiria hao aliyejitambulisha kwa jina la mama Imma amesema haelewi ni nini kilichotokea lakini alishangaa kushtushwa na kishindo cha kuanguka kwa basi hilo ila anamshukuru Mungu kutoka salama katika ajali hiyo.
Hadi mwandishi wetu anaondoka eneo la tukio majira ya saa 11 jioni majeruhi wote walikuwa wamepelekwa hospitalini na abiria wengine kuendelea na safari na polisi walikuwa hawajafika eneo la tukio, hivyo bado hatujapata uhakika ni abiria wangapi wamejeruhiwa ama pengine kumetokea kifo
CREDIT TO EDDY BLOG
Artikel Menarik Lainnya
Ajali imetokea Tunduma mkoani Mbeya maeneo ya Sogea Ajali imetokea Tunduma, hapa mkoani Mbeya maeneo ya Sogea katika matuta ya Shule ya Msing
BREAKING NEWS AJALI MBAYA INAYOHUSISHA MAGARI MATATU YATOKEA MUDA HUU MAENEO YA IGURUSI MBEYA. Picha zote na Mbeya yetu Blog
BREAKING NEWS MWILI WA MTU MMOJA AMBAYE NI ALBINO UMEKUTWA UMETUPWA MAENEO YA SEGEREA KINYEREZI HUKU UKIWA UMETOLEWA MACHO YOTE SAMAHANI KWA PICHA HIZI Inasadikiwa mtu huyu amekuja kutupwa eneo hili kutoka eneo ji
MBUNGE WA LUDEWA DEO FILIKUNJOMBE NA BABA WA JERRY SILAA WAFARIKI DUNIA R.I.P Jerry Silaa amepost Ujumbe huu akithibitisha kufariki kwa Mbunge Deo Filikunjombe pamoja na b
Rwanda, Morocco in sustainable urban development partnership Rwanda’s efforts to enhance urban development have been boosted following
MTEULE WA CCM JIMBO LA MBEYA MJINI AKABILIWA NA KESI YA JINAI Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM Mbeya Sambwee Shitambala Normal 0 false
EmoticonEmoticon