ARGENTINA NA UJERUMANI FAINALI KOMBE LA DUNIA 2014, UHOLANZI BYE BYE


Lionel Messi, Pablo Zabaleta, Martin Demichelis, Marcos Rojo, Lucas Biglia, Javier Mascherano, Rodrigo Palacio and Ezequiel Garay of Argentina celebrateARGENTINA imetinga fainali ya Kombe la Dunia baada ya kuifunga Uholanzi kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 Uwanja wa Sao Paulo nchini Brazil.Head-to-head: Ezequiel Garay and Robin van Persie collide in a painful mid-air collision
Sifa zimuendee kipa Romero aliyeokoa penalti mbili za Ron Vlaar na Wesley Sneijder na kuipeleka Argentina Fainali.
Arjen Robben na Dirk Kuyt pekee ndiyo walifunga penalti upande wa Uholanzi, wakati za Argentina zilikwamisha kimiani na Maxi Rodriguez, Sergio Aguero, Ezequiel Garay na Lionel Messi.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Cuneyt Cakir wa Uturuki, timu zote zilishambuliana kwa zamu na sifa ziwaendee walinzi na makipa wa timu hizo waliofanya kazi ya ziada kulinda nyavu.Flying Dutchman: Arjen Robben is sent tumbling by a slide challenge during the ill-tempered semi-final
Arjen Robben alikuwa mwiba mbele ya safu ya ulinzi ya Argentina- kadhalika na Lionel Messi alikuwa mwiba kwa safu ya ulinzi ya Uholanzi katika mchezo huo wa marudio ya fainali ya mwaka 1978.   Nasty: Georginio Wijnaldum raises his boot to Javier Mascherano after the Argentina man heads the ball clear, one of many moment of aggression in the match
Argentina sasa itamenyana na Ujerumani katika fainali ambayo jana iliwatoa wenyeji Brazil kwa mabao 7-1.
Kikosi cha Uholanzi kilikuwa: Cillessen, De Vrij, Vlaar, Martins Indi/Janmaat dk46, Kuyt, De Jong/Clasie dk62, Sneijder, Wijnaldum, Blind, Robben na Van Persie/Huntelaar dk96.
Argentina: Romero, Zabaleta, Demichelis, Garay, Rojo, Biglia, Mascherano, Lavezzi/Maxi Rodriguez dk101, Messi, Perez/Palacio dk81 na Higuain/Aguero dk82
Previous
Next Post »