Kuhusu kesi ya Mramba na Yona,hiki ndicho kilichoamuliwa na Mahakama leo.


BASIL YONA

Leo March 11 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewaruhusu kwenda kutibiwa nje ya nchi  Mawaziri Waandamizi wa zamani ambao ni Basil Mramba na Daniel Yona wanaokabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.

Matumizi hayo mabaya ya madaraka yanadaiwa  kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni 11.7  kwa kutoa msamaha wa kodi.

Uamuzi huo umetolewa leo mahakamani hapo na Jaji John Utamwa baada ya washtakiwa hao kuwasilisha maombi ya kwenda kutibiwa nje ya nchi ambapo Upande wa Jamhuri ulidai kuwa hauna pingamizi na maombi hayo.
Previous
Next Post »