Audio: Jay Z amtaja Lupita Nyong'o kwenye verse yake "Im on my Lupita Nyong'o..." Sikiliza Hapa


Lupita Nyong’o, muigizaji wa kike toka Kenya anaendelea kung’aa na kuwa mada
 ya kuzungumziwa 
hata na watu maarufu na sasa amemkuna kichwa rapper mkongwe Jay Z na ameamua
 kumuweka
 kwenye mistari ya shairi lake.


Kushinda tuzo kubwa ya Oscar kupitia filamu ya 12 Years A Slave ni kitu ambacho
 kimeyabadilisha
 kabisa maisha ya mrembo huyu na kumuweka rasmi kwenye orodha ya watu
 maarufu zaidi 
kwenye kiwanda cha filamu duniani kwa mwaka 2013/2014.
Jay Z amemtaja 

Lupita Nyong’o kwa kumpa sifa yeye na filamu ya 12 Years A Slave
 kwenye wimbo
 alioshirikishwa na Jay Electronica akiwa amefanya kama mtindo huru, wimbo unaitwa
 ‘We Made It’.
“I’m om my Lupita Nyong’o/ Stuntin on stage after 12 Years A Slave
This Ace of Spades look like an Oscar /Black tux, look like a mobster. Amerap Jay Z.
Kuna uwezekano kabisa kuwa Beyonce na Jay Z waliwahi kumzungumzia Lupita kwa
 mazuri kama

 wanafamili na ndio maana alimuingia akilini wakati anachora mistari hiyo.
Well, huenda tukasikia siku moja rais Obama ambaye ni rafiki mkubwa wa
 Jay Z akimtaja
 Lupita Nyong’o kwa mazuri.
Jay Z pia alimtaja Drake kwenye wimbo huo na kujibu kile ambacho Drake alikisema
 kuwa siku hizi
 Jay Z hawezi kurap bila kutaja angalau baadhi ya vitu vya sanaa ya rap (michoro n.k)
 wakati
 anazungumzia jinsi anavyopenda sanaa ya michoro.
Jay Z alieleza kuwa siku hizi kuna watu wanarap kuhusu vitu ambavyo hawafanyi tofauti na yeye anayerap kile anacho fanya.
“Sorry Mr. Drizzy for so much art talk/ Silly me, rappin’ ’bout sh-t that I really bought
While these rappers rap about guns that they ain’t shot/ And a bunch of other
 silly sh-t that
 they ain’t got.”

Usikilize hapa wimbo wa Jay Electrica ‘We Made It’:

Previous
Next Post »