Rais JK ametunuku kamisheni kwa maafisa wanafunzi wa jeshi 208 wa cheo cha Luten Ussu .


 Rais  Dr. Jakaya ametunuku kamisheni kwa maafisa wanafunzi wa jeshi 208 wa cheo cha Luten Ussu  waliohitimu mafunzo  yao katika chuo cha mafunzo ya kijeshi  TMA kilichoko Monduli mkoani Arusha .
Kabla ya kutunuku kamisheni kwa wahitimu hao wakiwemo 15 waliotoka nchi rafiki Mh rais Dr Jakaya   Kikwete ambaye pia ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama alikagua gwaride la wahitimu  hao ambalo lilipota mbele  yake na kutoa heshima.
Baada ya Mh Rais kutunuku kamisheni kwa wanafunzi hao wa kozi ya 53 ya mwaka mmoja ambao 5 wanatoka Uganda ,4 visiwa vya Shelisheli , 2 kutoka  Rwanda na 2 kutoka Swatzaland wanafunzi hao walikula kiapo cha utii kwa Mh rais.
Katika hafla ya kutunuku kamisheni hizo pamoja na kuhudhuriwa na wananchi walikuwepo viongozi wa  ngazi mbalimbali akiwemo waziri mkuu aliyejiuzulu Mh Edward Lowassa, waziri wa mambo ya ndani Mh  Shamsi Vuai Nahodha, mkuu wa majeshi general Davis Mwamunyange.
Wengine ni pamoja na makamanda wa ngazi mbalimbali za jeshi kutoka ndani na nje ya nchi  walioongozwa na general Mirisho Sarakikya, makatibu wakuu walioongozwa na katibu mku kiongozi  ,  pamoja viongozi na watendaji wa ngazi mbalimbali wakiwemo wakuu wa wilaya na mikoa  walioongozwa na mkuu wa mkoa wa Arusha bw Magesa Mulongo .
Previous
Next Post »