Katika
sehemu ya kwanza ya makala hii, nilielezea
mitazamo mbalimbali na misemo atumiayo binadamu kujikweza au
kujishusha,mojawapo ni methali isemayo “Ng’ombe wa masikini hazai” nilieleza
kwamba iwapo Ng’ombe wa masikini atatunzwa lazima azae tena naweza kuzaa
mapacha. Nilieleza kwa kifupi maendeleo ya ujasiriamali hapa Tanzania na
duniani kwa kifupi,aidha niligusia jinsi mataifa ya wenzetu yalivyochukua hatua
imara za kumkuza mjasiliamali na ndipo yakatokea mapinduzi ya viwanda.
Wenzetu
walitumia mbinu gani mpaka Ng’ombe wa maskini akazaa mapacha? Nitaeleza kwa
kirefu hapa chini.
Ikiwa mambo ni magumu,je unayatatua
vipi? Moja ya njia ya kuhakikisha kwamba Ng’ombe wetu anazaa ni kujifunza kuwa
watafiti na wachunguzi zaidi. Rais Kennedy wa Marekani wa enzi hizo alipata
kusema kwamba ukitaka kuendelea katika jamii jiulize malengo yako ni nini?
Eric
Hobsbawm, katika kitabu chake cha “How to Change the World:
Reflections on Marx and Marxism”anasisitiza kwamba mapinduzi ya viwanda na ujasiriamali
'yalianza' nchini Uingereza katika miaka ya 1780 na hayakuonekana
kikamilifu hadi miaka ya 1830 au 1840, ilhali T.
S. Ashton anaamini
kwamba ilifanyika, kwa kukadiria, kati ya mwaka wa 1760 na 1830. Baadhi ya
wanahistoria wa karne ya ishirini kama vile John
Clapham na Nicholas
Crafts wamedokeza
kuwa mchakato wa mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yalifanyika hatua kwa hatua
na kuwa neno mapinduzi halifai kuelezea yaliyofanyika. Hii bado ni mada
inayojadiliwa na wanahistoria.
Mapato ya kiujumla ya Nchi ya kila mtu kwa upana yalikuwa imara
kabla ya Mapinduzi ya Viwanda na kuibuka kwa uchumi wa kisasa wa kibepari. Mapinduzi ya
viwanda yalianzisha zama za ustawi
wa kiuchumi na ulilenga
kuleta mapato ya kila mtu katika nchi zenye uchumi wa
kibepari. Wanahistoria wanakubaliana kwamba Mapinduzi ya Viwandani yalikuwa
mojawapo ya matukio muhimu sana Kihistoria.
Arnold
Toynbee anayetambulika kama mwasisi wa Mapinduzi
ya Viwandani, na ambaye hotuba zake zilizotolewa mnamo mwaka wa 1881
zilikuwa na maelezo ya kina. Vyanzo vya Mapinduzi ya Viwandani ni vigumu
kuelezea na vinabaki kuwa swala la kujadiliwa, huku baadhi ya wanahistoria
wakiamini kuwa Mapinduzi hayo yalikuwa sehemu ya mabadiliko ya kijamii na
kitaasisi yaliyosababishwa na kuisha kwa Ubwana nchini Uingereza baada ya Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya
Uingereza katika karne
ya 17.
Mapinduzi ya Kilimo ya Uingereza yalifanya uzalishaji wa chakula kuwa
rahisi zaidi na kutotegemea wafanyakazi wengi, hivyo kulazimisha idadi ya watu
ambao hawengeweza kupata kazi katika kilimo wajiunge na viwanda vya karakana,kwa mfano ushonaji, na baada ya
kipindi kirefu wakajiunga na miji na viwanda vilivyokuwa
vimejengwa upya wakati huo. Upanuzi
wa kikoloni wa karne ya 17
ulioambatana na maendeleo ya biashara ya kimataifa, kuundwa kwa masoko
ya kifedha na kukusanywa
kwa mtaji pia zinatajwa kama sababu, kama tu mapinduzi ya kisanyansi ya karne ya 17.
Kuwepo kwa soko kubwa la ndani pia unapaswa kutiliwa
maanani kama chanzo muhimu cha Mapinduzi ya Viwandani , hasa katika kuelezea
mbona yakafanyika nchini Uingereza. Katika mataifa mengine, kama vile Ufaransa,
masoko yalipasuliwa na kimkoa, mikoa ambayo mara nyingi ilituza ushuru n a kodi kwa bidhaa
zilizouzwa miongoni mwao.
Serikali kuwapa wavumbuzi uwezo wa kipekee wa kuuza ambao ulipimwa chini ya mfumo uliokuwa
ukiendelezwa wa patenti ( Katiba ya Uwezo wa Kipekee wa
Kuuza 1623) inatambulika
kama sababu muhimu.Matokeo ya patenti, mabaya na mazuri, ya maendeleo ya
viwanda yanaonyeshwa wazi katika historia ya injini ya mvuke, teknolojia muhimu
ya kuwezesha mapinduzi hayo.
Kama malipo ya kuonyesha wazi mbele ya umma jinsi kifaa
kilichovumbuliwa kilivyofanya kazi mfumo wa patenti uliwalipa wavumbuzi kama James Watt kwa kuwaruhusu
kuwa na uwezo wa kipekee wa kuunda injini za kwanza za mvuke, hivyo basi
kuwalipa wavumbuzi na kuongeza kasi ya maendeleo ya kiteknolojia.
Hata hivyo uwezo wa kipekee wa kuuza kawaida husababisha
madhara yanayoweza kuondoa, au hata kuzidi kwa umbali, matokeo mazuri ya
kufanya uvumbuzi uwe wazi mbele ya umma na kuwalipa wavumbuzi.
Uwezo wa kipekee wa Watt wa kuunda injini za mvuke huenda
kulizuia wavumbuzi wengine, kama vile Richard
Trevithick, William
Murdoch au Jonathan
Hornblower, kuunda injini
za mvuke bora zaidi, hivyo basi kuchelewesha maendeleo ya mapinduzi ya
viwandani kwa takriban miaka 16.
Baadhi ya wahistoria kama vile David
Landes na Max Weber wanaashiria mitazamo mbalimbali nchini Uchina na Ulaya
na kuamuru mahali ambapo mapinduzi yalitokea. Dini na imani za Ulaya zilikuwa
haswa chanzo cha Ukristo
wa Kiyudea, na dhana za
Kigiriki. Jamii ya Kichina ilikuwa na msingi wake katika watu kama vile Confucius, Mencius, Han
Feizi (Matendo
bila Imani), Lao
Tzu (Utao), and Buddha (Ubudha).
Watu wa Ulaya walipoamini kuwa ulimwengu ulitawaliwa na
sheria za kimantiki na za milele, watu wa Mashariki, waliamini kuwa ulimwengu
ulibadilika kila uchao na, kwa Wabudha na Watao, haungeweza kueleweka
kimantiki.Kwa sisi Afrika tuliamini kwamba dunia ama ulimwengu ni matokeo ya
nguvu inayozidi nguvu zote.
Mjadala kuhusu mwanzo wa Mapinduzi ya Viwanda pia
unahusisha jinsi Uingereza ilivyozitangulia inchi zingine na
kuzishinda kwa mbali. Kuna watu ambao wamesisitiza umuhimu wa rasilimali za
kiasili au za kifedha ambazo Uingereza ilipokea kutoka nchi nyingi za nje ilizozitawala au faida
kutokana na biashara
ya utumwa ya Uingereza,
kati ya Afrika na eneo la Karibiani, iliyosaidia kuendesha uwekezaji wa
viwandani.
Imedokezwa kuwa, mbali na hayo, kuwa biashara ya Utumwa
na mashamba makubwa ya Uhindi ya Magharibi yalitoa 5% pekee ya mapato ya
kitaifa ya Uingereza wakati wa miaka ya Mapinduzi ya Viwandani. Ingawa utumwa
ulikuwa chanzo cha faida cha kiasi kidogo cha kiuchumi nchini Uingereza wakati
wa Mapinduzi ya Viwandani, mahitaji kutoka eneo la Karibiani yaliambatana na
12% ya pato la viwanda vya Uingereza.
Kwa upande mwingine, biashara kufanywa huru zaidi
kutokana na msingi mkubwa wa wabepari huenda ikawa uliruhusu nchi ya Uingereza
kutengeneza na kutumia maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia vizuri zaidi
kuliko nchi zilizokuwa na milki zenye nguvu zaidi, hasa Uchina na Urusi.
Uingereza iliinuka kutoka Vuta vya Kinapolioni kama taifa pekee Ulaya ambalo halikuwa
limeharibiwa na utumizi mbaya wa fedha na kuharibika kwa uchumi, na ikiwa meli
za kibiashara kubwa za kipekee (Meli za kibiashara za Ulaya zilikuwa
zimeharibiwa katika kipindi cha vita na Jeshi la Uingereza la Wanamaji).
Nadharia nyingine ni kuwa Uingereza iliweza kufanikiwa
katika Mapinduzi ya Viwandani kwa sababu ya kuwa na rasilimali muhimu. Nchi ya
Uingereza Ilikuwa na idadi kubwa ya wakazi katika kila eneo mraba
ikilinganishwa na umbo lake ndogo la kijiografia. Kupimwa kwa ardi
iliyotumika na kila mtu na mapinduzi ya kilimo yanayohusiana na hili
kulisababisha kupatikana kwa wafanyikazi kuwe rahisi.
Hali tulivu ya kisiasa nchini Uingereza tangu miaka ya
1688, na nia zaidi ya jamii ya Kiingereza kukubali mabadiliko (ikilinganishwa
na nchi zingine za Ulaya) inaweza pia kusemwa kuwa sababu iliyowezesha
Mapinduzi ya Viwandani. Kwa sehemu kubwa, kwa sababu ya Harakati ya Kufungiwa,
watu maskini waliangamizwa kama chanzo kubwa cha upinzani dhidi ya kuenea kwa
viwanda, na watu wa madaraja ya juu waliendesha maslahi ya biashara
yaliyosababisha watu wa kwanza katika kuondoa vikwazo dhidi ya ukuaji wa
ubepari (Wazo hili pia limedokezwa katika kitabu cha Hilaire
Belloc, Nchi
ya Kitumishi.)
Nadharia nyingine ni kwamba mafanikio ya Waingereza
yalikuwa kwa sababu ya kuwepo kwa daraja la Kijasiriamali ambalo
liliamini kuwa kulikuwa na maendeleo, teknolojia na kazi ngumu. Kuwepo kwa
daraja hili mara nyingi huusishwa na maadili ya kazi ya Kiprotestanti (tazama Max Weber) na hasa hadhi ya Wabatizi na madhehebu
yanayopingana nao ya Kiprotestanti, kama vile Wakweka na Wapresbiteri ambazo
zilikuwa zimenawiri wakati wa Vita vya Wenyewe kwa Wenyewe vya
Uingereza.
Wanahistoria wakati mwingine hutazama kipengele hiki cha
kijamii kuwa muhimu sana, pamoja na hali ya uchumi wa mataifa yanayohusika.
Ingawa wanachama wa madhehebu haya walitengwa mbali na duru fulani za
kiserikali, walitazamwa na Waprotestanti wenzao kama, kwa kiwango kidogo, na
wengi katika daraja
la kati, wakopaji pesa
wa jadi au wanabiashara wengine. Kutokana na kuvumilia huku, kiasi na
usambazaji wa mtaji, njia ya kimaumbile ya watu wenye nia ya ujasirimali ya
haya madhehebu ingekuwa kutafuta nafasi mpya katika teknolojia zilizoundwa
wakati wa mapinduzi ya kisayansi ya karne ya 17.
Kwa mujibu wa muundo wa kijamii, Mapinduzi ya Viwandani
yalishuhudia ushindi wa watu wa daraja
la kati ya wanaviwanda
na wafanyabiashara ambao waliwashinda daraja la watu lenye ardhi ya mabwana
wakubwa.
Watu wa kawaida walipata fursa nyingi zaidi za kufanya
kazi katika viwanda vipya vya kutengeneza bidhaa, lakini hizi zilikuwa chini ya
mazingira magumu ya kikazi yakiwa na masaa marefu ya kazi yaliyotawaliwa na
mbio za kufanya kazi za mashine. Hata hivyo, hali ngumu za kikazi yalikuwa
miaka mingi kabla ya ujio wa Mapinduzi ya Viwandani kufanyika. Jamii ya kabla
ya viwanda haikuwa na mabadiliko mengi na mara nyingi ilikuwa na uhasama
mwingi—watoto
kufanya kazi, hali hafu za
maisha, na masaa marefu yalikuwa kwa wingi hata kabla ya Mapinduzi ya
Viwandani.
Nimeelezea kwa kirefu hatua mbalimbali za mapinduzi ya
viwanda huko ulaya ili uamini kwamba hata sisi watanzania tunaweza kabisa,
waingereza wa karne ya 15 waliweza na Ng’ombe wao akazaa mapacha,inakuwaje
kwetu wasizae?
Mwandishi, Fidelis Butahe aliwahi kusema kwamba, huwezi kuiweka Tanzania katika kundi la nchi maskini zaidi
duniani hata siku moja. Kwa maana kwamba
Ng’ombe wa maskini naweza akazaa tena uzao wake unaweza kuwa mapacha na
kumshangaza mfugaji. Hii ni kutokana na ukweli kuwa ina utajiri mkubwa wa
rasilimali, ingawa wananchi wake bado ni maskini wa kutupwa. Swali la kujiuliza
hapa ni je tatizo ni nini? Utangundua kwamba tukiachana na imani potofu Ng’ombe
wetu atazaa mapacha.Na ndivyo ilivyo kwenye ujasiriamali weka mikakati ya aina
ya ujasiriamali unaotaka na Ng’ombe wako atazaa mapacha.
Tatizo kubwa letu
na penginepo duniani ni kuwa, na baadhi
ya viongozi hasa wale wa kisiasa na watu
wa kada ya kati (middle class) na wananchi ni kuwa na imani potofu na kujilisha
imani za kimasikini kwamba pasipo ajira hakuna kinachofanyika.
Juzi usiku kuna
msomaji wa makala ya uchumi na biashara aliniambia kwamba, watu wanaojiita
wasomi,nivigumu sana kufanya biashara za kisomi kwasababu wao niwaoga wa
kuthubutu mambo, wanashindwa kujaribu.Alienda mbele kwa kusema kwamba, hapa
Iringa mjini makampuni mengi, na majengo makubwa yanamilikiwa na watu ambao
hajasoma ama wana elimu tu ya kawaida.
Maggid Mjengwa
ambae ni ‘mentor’ wangu alipata kusema kwamba,
“Tumekuwa watu wa kulalamika sana. Na tumemwachia Mungu jukumu la
kutukomboa kutoka kwenye umasikini wetu. Hapana, Mungu hausiki na umasikini
wako, unaosababisha Ng’ombe wako asizae. Jukumu la kwanza la kujikomboa kutoka
kwenye umasikini ni lako mwenyewe. Tumeendekeza imani potofu zilizozagaa
mitaani za Free mason na zinazoandikwa kwenye magazeti ya udaku kila leo
Na hakuna njia ya mkato, bali ni kufanya kazi,
kufanya kazi na kufanya kazi. Tufanye mapinduzi kama waingereza wa miaka hiyo.
Achana na ndoto za kuamka na kuvuna mamilioni.Inakuwaje mwanadamu mmoja awe na
muda na mwingine asiwe nao? Kuwa au kutokuwa na muda, inatokana na mipangalio
yako ya maisha. Binadamu unapaswa kuwa na bajeti ya muda wako.
Ni jinsi unavyotumia muda wako, jinsi
unavyopangilia mambo yako, imani yako kuhusu pesa,kushabikia siasa za marekani
na michezo ya kuigiza na mambo mengine ya kufikirika, kuliko mambo, mwisho wa siku unaishia kutamka kauli tata za
NG’OMBE WA MASKINI HAZAI, sasa kama
halishwi na hatunzwi atazaa kweli? Jiulize.
Maisha ni magumu sawa,mifumo ya nchi
ni mibovu sawa,uchumi wa nchi unaporomoka sawa lakini haiwezi kuwa na madhara
katika roho ya binadamu aliyeamua maisha yake.
Mambo ni mengi yanayoweza kuturudisha nyuma lakini ukirudi nyuma ni maamuzi yako wewe na si mambo yanayokuzunguka. Au kiongozi wako wa kisiasa.
Mambo ni mengi yanayoweza kuturudisha nyuma lakini ukirudi nyuma ni maamuzi yako wewe na si mambo yanayokuzunguka. Au kiongozi wako wa kisiasa.
Mawasiliano:
meshackmaganga@gmail.com
EmoticonEmoticon