Wafanyabiashara
mbalimbali wa kariakoo leo wameingia kwenye Mgomo kuishinikiza serikali
kupunguza bei ya mashine za TRA ambazo zipo kwa ajili ya kutoa risiti.
Mashine
hizo ziitwazo Electronic Fiscal Device[EFD]
wamezigomea wakidai zinauzwa bei kubwa na sababu nyingine ni ile asilimia
inayokatwa kwenye kila bidhaa inayouzwa ambayo ni asilimia 18%.
Huyu ni mmoja kati ya wafanyabiashara wa
kariakoo ambaye pia ni msanii wa Bongo fleva anaitwa sideboy.
Katika pitapita zangu hili ni duka pekee
nililolikuta wazi kwenye barabara ya uhuru lakini niliporudi mara ya pili muda
mfupi nikakuta limefungwa.
Hili duka la Home shopping centre lipo barabara
ya Uhuru nalo lilikuwa limefungwa.
Wafanyabiashara mbalimbali wakiwemo raia
wa nchi ya Congo hapa.
Hapa ni Wafanyabiashara wakiwa wanajadili
kuhusu huu mgomo ambao haujajulikana utaisha lini.
picha
zote zimepigwa na millardayo.com
EmoticonEmoticon