Mmoja wao aliangua kilio na kuanguka baada ya kutangazwa kwa hukumu dhidi yao .
Msichana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 aliumizwa sana na baada ya wiki moja alifariki kutokana na majeraha .
Karibu miezi 9 baada ya ubakaji ulioitikisa India, jaji ametoa hukumu kwa wanaume wote wanne ambao tayari walikuwa wamepatikana na hatia ya uhalifu .
Wendesha mashtaka walikuwa wamewaombea hukumu ya kifo wakisema ingetoa ishara muhimu kwamba uhalifu wa aina hiyo hautakubalika kamwe .
Familia ya mwanamke huyo pia waliomba wanaume hao wanyongwe .
Lakini mawakili watetezi wa wanaume hao walipinga mapendekezo ya hukumu ya kifo , wakisema wateja wao hawakuwa na rekodi za uhalifu awali na kwamba wanastahili kusamehewa .
Next
« Prev Post
« Prev Post
Previous
Next Post »
Next Post »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
EmoticonEmoticon