Meek Mill amjibu Kendrick Lamar aliyejipa jina ‘Mfalme wa New York’ kwenye wimbo mpya wa Big Sean

Internet jana ilichemka kwa moto aliouanzisha Kendrick Lamar kwenye wimbo alioshirikishwa na Big Sean, Control ambapo pamoja na kuwataja rappers kibao kuwa atahakikisha anawapoteza wote kwenye ramani, alijipa cheo cha Mfalme wa New York.

Meek Mill ambaye alitajwa pia amejibu lakini amesema alichokiongea Lamar si tusi na wala hawezi kutoa ngoma ya kumdiss.

“Ni hakika hakutukana. Kendrick Lamar,sidhani kama alikuwa anajaribu kututukana. Wote tunafahamiana vizuri.Kuna majina mengi yaliyotajwa. Napenda game za aina hiyo. Sidhani kama ametukana. Ni kitu cha ushindani. Naishi kwa ushindani. Kila mtu anayenifahamu anajua kuwa huwa sikubali kushindwa. Sitatoa wimbo wa kumdiss Kendrick Lamar. Lakini kama anataka kushindana, tutaenda kufurahi,” alisema Meek Mill.

Previous
Next Post »