Waziri Samuel Sitta afungua rasmi baraza la vijana la taifa la katiba.


PIX 1

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo Mashariki Mhe. Samuel Sitta akiwahutubia vijana (hawapo pichani) waliohudhuria wakati wa ufunguzi wa Baraza la Vijana la Taifa la Katiba lililofanyika jana  jijini Dar es Salaam.

PIX 3

Bw. Julius Toneshe aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo akiongea wakati wa ufunguzi wa Baraza la Vijana la Taifa la Katiba jana  jijini Dar es Salaam.

 PIX 5

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Vijana ya Youth Coalition (TYC) Lenin Kazoba (kushoto) akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Samuel Sitta ( kulia) wakati wa ufunguzi wa Baraza la Vijana la Taifa la Katiba lililofanyika jana  jijini Dar es Salaam. 

PIX 6

Meneja Mipango wa Taasisi ya Vijana ya Youth Coalition (TYC) Bi. Rahma Bajun akiongea baada ya kumkaribisha mgeni rasmi Mhe. Samuel Sitta kwa ajili ya kutoa hotuba yake na kufanya ufunguzi rasmi wa Baraza la vijana la Taifa la Katiba jijini Dar es Salaam.

PIX 7

Mratibu wa Taasisi ya Vijana ya Tanzania Youth Coalition Rebecca Gyum akiongea wakati wa ufunguzi wa Baraza la Vijana la Taifa la Katiba lililofunguliwa rasmi na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Samuel Sitta.

PIX 9

Baadhi ya washiriki ambao ni vijana mbalimbali kutoka Wilaya 50 za mikoa yote Tanzania wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi Mhe. Samuel Sitta (hayupo pichani) wakati akitoa hotuba kwa vijana hao.  Salaam.

PIX 10

PIX 8

PIX 12

Picha ya pamoja katikati ni Waziri wa Ushirkiano wa Afrika Mashariki Mhe. Samuel Sitta, kushoto kwake ni Bw. Julius Toneshe na Meneja Mipango wa TYC Bi. Rahma Bajun. Wa kwanza kutoka kulia kwake ni   Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Vijana ya Youth Coalition (TYC) Lenin Kazoba na Meneja wa Restless Development. (picha zote na Benedict Liwenga-Maelezo).

Waziri wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo Mashiriki Mhe. Samuel Sitta amewaasa vijana kutoa maoni yao juu ya uundwaji wa Katiba mpya ambayo haijengi mifumno ya serikali ya Udikteta, ubinafsi na ambayo haitaibebesha mzigo Serikali.

Mh. Sitta amesema hayo akifungua rasmi Baraza la Vijana la Taifa la Katiba lililoandaliwa na Taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Coalition (TYC) kwa kushirikiana na Restless Development-UNFPA na ILO, lililojumuisha vijana 120 kutoka Wilaya 50 za mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani na ambao wanatoka katika mashirika mbalimbali, asasi, jumuiya na vikundi mbalimbali vya vijana.

Waziri Sitta amewaasa vijana kuwa TYC pamoja na vijana wengine nchini wanalojukumu kubwa la mapambano dhidi ya kupinga ulafi katika mambo ya uongozi, udikteta pamoja na ubinafsi kwani vinailetea mzigo serikali.

Ameongeza kuwa vijana nchini wanatakiwa wawe Wanaharakati katika kujali maadili mema na kusimamia kwa dhati pamoja na kupigania haki na usawa nchini.

Aidha, kwa upande mwingine Waziri Sitta amevishukuru vyombo vya habari kwa mchango wake mkubwa wa kufanya kazi ya kuhabarisha umma na pia ameipongeza taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Coalition kwa kuandaa baraza hilo kwa vijana wenzao, kwani litawasaidia kutambiua mambo ya msingi yanayohitajika kuwepo katika Katiba mpya ya nchi.

Waziri Sitta amesema kuwa katika kutoa maoni juu ya Katiba mpya, vijana wanaweza kupata katiba yenye manufaa mazuri au yenye athari kwa maisha yao, hivyo amewaasa vijana wote watumie fursa wanazozipata kupitia baraza hilo lililoandaliwa na TYC, ili waweze kusikika katika mambo yanayohitajika katika Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taasisi ya vijana ya Tanzania Youth Coalition ni moja ya taasisi iliyoundwa kwa malengo ya kuhakikisha kuwa vijana wanashiriki na kushirikishwa katika mchakato wa kuunda katiba mpya ulioanza mwaka jana hapa nchini.

Previous
Next Post »