Watu zaidi ya 75 wamekufa nchini Hispania kufuatia ajali mbaya ya treni kuacha njia na kupinduka.


Rescue workers pull victims from a train crash near Santiago de Compostela, northwestern Spain, July 24, 2013. At least 35 people died after a train derailed in the outskirts of the northern Spanish city of Santiago de Compostela, the head of Spain's Galicia region, Alberto Nunez Feijoo, told Cadena Ser radio on Wednesday.  A woman who was close to the site of the accident told the radio station that she had first heard a loud explosion and then seen the train derailed.  REUTERS/Oscar Corral (SPAIN - Tags: DISASTER TRANSPORT TPX IMAGES OF THE DAY)

Watu takriban 77 wamekufa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa kati ya abiria 218 baada ya treni moja ya abiri kuacha njia na kuanguka kaskazini magharibi mwa Hispania.

Mabehewa yote 8 ya treni hiyo iliyokuwa ikitoka Madrid kuelekea Ferrol yameanguka  karibu na mji wa Santiago de Compostela.

Taarifa za vyombo vya habari zinasema huenda treni hiyo ilikuwa ikienda kwa mwendo kasi wa mara mbili ya kipimo chake katika eneo lenye kona.

Maafisa mjini humo hawajasema lolote kuhusiana na chanzo cha ajali hiyo huku wachambuzi wa mambo wakisema ni ajali mbaya zaidi ya treni kutokea nchini Hispania katika kipindi cha miaka 40.

Ajali kubwa ya treni kuwahi kutokea nchini humo ilikuwa mwaka 1972 wakati watu 77 walipokufa baada ya treni kuacha njia huko Andalusia eneo la kusini.

Previous
Next Post »