Msanii Z anto afiwa na mama yake mzazi



Kwa taarifa zilizotufikia hivi punde ni kuwa msanii Z Anto amefiwa na mama yake mzazi masaa machache yaliyopita, akiwa katika hospitali ya muhimbili ambapo alikuwa amempeleka masaa mawili yaliyopita.
Nw nipo muhimbili nmemleta mama hali yake c nzuri kabisa, ingawa kuumwa sio kufa ila kwa hali aliyonayo lolote laweza kutokea. naomben dua zenu ndugu zangu.
akiongea na blog hii dakika chache zilizopita Z Anto amesema Mama yake, alikuwa anasumbuliwa na cancer ya ini kwa muda mrefu, lakini kwa takribani miezi miwili iliyopita hali yake ilianza kubadilika, na leo hii walimpeleka hospitali ya taifa ya Muhimbili, ambapo alifariki muda mchache baadae.
Pole sana kwa Z Anto, familia nzima, ndugu jamaa na marafiki kwa msiba huu uliowafika.
Mungu ailaze roho ya marehem mahali pema peponi ameen.
Previous
Next Post »