BREAKING NEWS: VURUGU ZAIBUKA KAWE DAR, WANANCHI WAZINGIRA KITUO CHA POLISI



Risasi zinarindima! Ni baada ya raia mmoja kupewa kichapo hadi kufariki.

Updates zitafuata

- Gari la Polisi (Difenda) limevunjwa vioo na wananchi wenye hasira kali
- Polisi wameelemewa, wameongeza nguvu ya gari la washawasha
Quote By MTAZAMO
Wanabodi,

Nimepata taarifa ya vurugu huko Kawe na wananchi kuzingira kituo cha polisi! nimechungulia humu sijaona post juu ya hili nikaona nitoe taarifa ili wenye taarifa kamili watujulishe maana chanzo changu hakikuwa na taarifa za uhakika wa chanzo cha vurumai hizo!!

Inasemekana mwanajeshi alikodi bajaji aliposhuka hakuona simu yake akatuhumu kuiacha kwenye ile bajaji hivyo yule askari akaita wanajeshi wenzake na kuanza kupiga madereva wa bajaji hadi dereva mmoja akapoteza maisha.
 
 
Quote By platozoom View Post
Ndiyo nami niko Mbezi kuna mabomu ya machzi na risasi zinasikika.

Chanzo ni wananchi kadhaa jana wakiwa kwenye kikao cha kilevi kutofautiana na Mwanajeshi mmoja na kuzuka vurugu ndogo. Leo wanajeshi wamepita mtaani kuwatafuta wabaya wao, Wananchi walipowaona wakaanza kukimbia, kando walimkuta kijana dereva wa bajaji, mmoja wa askari akaaanza kumpa kipigo (kimsingi hakuwamo kwenye ugomvi) na kupoteza maisha.

Baada ya hilo Wanachi wakamkimbiza yule mwanajeshii mpaka kwake na kumkabidhi Polisi. Lakini wakati wa sekeseke
la msiba Raia wakasema haiwezekani atuulie Kijana mwenzetu. Wakaandamana hadi kituoni ili kumchomoa mbaya wao.

Na hali ya mambo ndiyo ikawa hivyo.
 
CHANZO JAMII FORUM
Previous
Next Post »