Jumla ya Askari  10 wa jeshi la Wananchi wa kambi ya 44KJ Mbalizi Wilaya ya Mbeya wanashikiliwa na jeshi lapolisi kwa tuhuma za kuhusika na kifo cha Petro Sanga (25) mkazi wa chapakazi Mbalizi aliyeuwawa kwa kuchomwa kisu shingoni na mdomoni.
 
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athuman alisema kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 18,2012 majira saa 3:00 usiku katika grocery iitwayo Vanenemwe ambapo marehemu alikuwa katika gocery hiyo alipochomwa kisu shingoni na mdomoni na kufariki dunia alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospiali teule ya Wilaya ya Ifisi Mbalizi.

 Akielezea tukio hilo Kamanda Athuman alisema kikundi kinachodakika kuwa ni wanajeshi wa jeshi la Wananchi 44KJ  kambi ya Mbalizi  walivamia katika baa ya iitwayo Power Night Club ambamo awali alikuwepo marehemu wanajeshi hao walianza kuwashambulia wananachi kwa kuwapiga ngumio na mateke,mikanda.marungu,sime na mapanga.

 
Alisema kuwa marehemu  alijaribu kuokoa uhai wake kwa kukimbia toka eneo hilo hadi katika grocery hiyo lakini watu hao walimkimbiza hadi eneo hilo na kumjeruhi vibaya kwa kumchoma kisu shingoni na mdomoni.

 
 Kamanda Athumani alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni kulipiza kisasi  kufuatia askari jeshi mmoja aliyetambulika kwa jina  la Godfrey Matete wa kikosi cha 44KJ Mbalizi kupigwa na walinzi wa kilabu cha pombe za kienyeji kiitwacho DDC kilichopo Mbalizi waliokuwa lindoni novemba 17,2012 majira ya saa 01:30 usiku.

 Alisema Mwanajeshi huyo alitoa taarifa katika kituo kidogo cha polisi cha mbalizi ambapo alifungua kesi na kupatiwa hati ya matibabu (PF3) kwa ajili ya kwenda kupata matibabu hospitalini na walinzi wanne walikamatwa na polisi kuhusiana na tukio hilo.
 
Aidha alisema kuwa katika siku hiyo watu wengine sita walijeruhiwa kwa kupigwa sehemu mbali mbali za miili yao na wanaodaiwa kuwa ni askari wa JWTZ na kupatiwa hati ya matibabu na kati yao watatu walilazwa katika hospitali teule ya ifisi .

Alisema kuwa katika vurugu hizo mali zawatu ziharibiwa ambazi ni pamoja na gari T.106 AWB iana ya Toyota Vista mali ya Paulo Maximililian iliyokuwa imevunjwa kioo cha mbele,gari T884 auu Toyota Cresta mali ya Alile Godfrey lilivunjwa Side Mirror upande wa kulia.

Kamanda Athuman alisema kuwa Mwili wa marehemu  ulifanyiwa uchunguzi  na daktari wa serikali na kisha kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajiliya taratibu za mazishi na kwamba uelelezi wa tukio hilo unaendelea  kufanyika.

Kamanda huyo ametoa wito kwa jamii kuepuka tabia ya kujichukulia sheria mkononi na pindi wanapotendewa isivyo halilali ni vizuri kutoa malalamiko yao katika mamlaka husika na ametoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki  wa marehemu Petro Sanga  kwa msiba mzito uliowakuta  na kuwataka kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu walichonacho.
Previous
Next Post »