JESHI la polisi Mkoani Mbeya limewataka wananchi kutoa ushirikiano wa kuwafichua watu wanaojihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya aina ya bangi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake kutokana na athari zinazojitokeza kwa vijana.
 Akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani mbeya Athuman diwani alisema kuwa kumekuwa na tabia ya wananchi kujihusisha na kilimo cha bangi na uuzaji katika wilaya ya chunya na hivyo kupelekea kushamili kwa biashara hiyo kwa kipindi cha hivi karibuni.

Aidha alimtaja mkazi wa kijiji cha makongorosi wilayani chunya mkoani mbeya Gineneka Charles(18) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na gramu 500 za bangi.

 Diwani alisema kuwa mtuhumiwa huyo alipohojiwa alikiri kujihusisha na biashara na bangi na kwamba anatarajia kufikishwa mahakani wakati wowote kujibu tuhuma zinazomkabili.
Awali katika tukio la pili watu wanne wanashikiliwa na polisi wakazi wa kijiji cha madibila wilayani mbarali mkoani mbeya kwa tuhuma za kupata na nyara za serikali

 Diwani aliwataja wanaoshikiliwa na kufikishwa mahamkamani kuwa ni

 Kelius mhanga(40) msafiri njiwa (33) charles kapemba(25) na martin Musinge (28 ) alisema watuhuumiwa wote kwa pamoja walikamatwa na polisi waliokuwa doria wakiwa na nyama ta tembo kilo 10, nyati kilo 15 na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Previous
Next Post »