RAIS
 John Magufuli leo anatarajiwa kupokea taarifa ya zoezi la uhakiki wa 
vyeti kwa watumishi wa umma katika Ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.
Taarifa
 iliyotolewa jana na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais katika 
Ikulu Ndogo ya Chamwino Dodoma, Jaffar Haniu ilisema taarifa hiyo 
itawasilishwa kwa Rais Magufuli na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, 
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki.
Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma liliendeshwa na Serikali kuanzia Oktoba, 2016. 
Hivi
 karibuni wakati akifungua rasmi nyumba mpya za makazi ya wanafunzi wa 
Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Rais Magufuli alisema anasubiri ripoti 
kuhusu watumishi wa umma wenye vyeti feki wapatao 9000.
“…Kwa
 hiyo mnaweza mkaona shida zilizopo katika nchi hii, huku wafanyakazi 
hewa karibu 19,000, wanafunzi hewa ni zaidi ya 56,000, kila mahali 
unapokwenda ni matatizo, lakini ni lazima niyatatue matatizo kwa sababu 
mlinichagua kwa ajili hiyo,” alisisitiza Rais katika hotuba yake hiyo.


EmoticonEmoticon