Sergio Aguero aweka rekodi Ligi Kuu Uingereza

Sergio Aguero
Sergio Aguero
Mshambuliaji Sergio Aguero alifunga goli katika kipigo cha 4-1 cha Manchester City kutoka kwa Liverpool.
Kwa sasa Kun Aguero anaongoza katika Ligi Kuu Uingereza kwa kuwa na magoli 85 kama mchezaji anayetoka Amerika Kusini.
Carlos Tevez
Carlos Tevez
Raia huyo wa Argentina, 27, amempiku mwenzake Carlos Tevez mwenye magoli 84.
Tevez aliwahi kuzichezea West Ham, Manchester United pamoja na Manchester City.
Luis Suarez
Luis Suarez
Wa tatu ni Luis Suarez mwenye magoli 69 aliyecheza misimu mitatu na nusu Liverpool kabla ya kutimkia Barcelona mwaka 2014.
Gus Poyet naye kutoka Uruguay anashika nafasi ya nne kwa kuwa na magoli 54.
Gus Poyet (shati jeupe)
Gus Poyet (shati jeupe)
WAFUNGAJI 10 WA AMERIKA KUSINI KUWAHI KUCHEZEA LIGI KUU UINGEREZA
Sergio Aguero Argentina-85
Carlos Tevez Argentina-84
Luis Suarez Uruguay-69
Gus Poyet Uruguay-54
Nolberto Solano Peru-49
Juan Pablo Angel Colombia-44
Hamilton Ricard Colombia-31
Juninho Brazil-29
Hugo Rodallega Colombia-29
Carl Cort Guyana-28
 print
Previous
Next Post »